Advertise here

TCRA: Idada ya utumiaji wa Internet yaongezeka

Kasomi

JT Founder
1760903625246.jpg

📌Huduma ya intaneti inaonesha kuongezeka utumiaji kutoka milioni 54.1 mwezi Juni 2025 hadi kufikia milioni 56.3 mwezi Septemba 2025 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 4.1.

Kwa mujibu wa ripoti ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano ya robo mwaka inayoishia Septemba 2025 inaonesha idadi ya utumiaji wa intaneti inatokana na laini/waya ambazo zimetumia huduma ya Intaneti angalau mara moja katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, bila kujali teknolojia iliyotumika (FTTX, 2G - GPRS na EDGE, 3G, 4G, au 5G).

Ripoti hiyo imefafanua kuwa huduma ya intaneti kwa njia ya simu ya mkononi inapendelewa zaidi (99%) ikilinganishwa na huduma ya intaneti isiyohashimishika.

Kuongezeka kwa utumiaji wa intaneti unatokana na ubora wa huduma na miundombinu inayowezesha upatikanaji wa mawasiliano kwa wananchi.
 
Back
Top