Advertise here

Mwanamuziki Cool James aka Mtoto wa Dandu Akiwa na Wadau Joseph Kusaga na Kinjeketile Kingunge Ngombale Mwiru Jijini Dar Es Salaam Miaka 2000

Kasomi

JT Founder
MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA MWANAMUZIKI COOL JAMES AKA MTOTO WA DANDU, MWASISI WA TANZANIA MUSIC AWARDS
1773931690900 (1).jpg

Pichani ni wadau wakubwa wa muziki nchini, toka kushoto Mtoto wa Dandu, Joseph Kusaga na Kinjeketile Kingunge Ngombale Mwiru miaka ya 2000.

Jina lake halisi lilikuwa James Dandu Maligisa, maarufu kama Cool James au Mtoto wa Dandu. Alizaliwa mwaka 1970 mjini Mwanza, Tanzania, na baadaye akaishi Stockholm, Sweden, ambako ndiko ndoto yake ya muziki ilianza kuchanua.

Akiwa huko Sweden alikumbana na changamoto za lugha na kujikuta akielekeza nguvu zake kwenye muziki kama njia ya kujieleza na kutambulika.

Mwaka 1988 alianza rasmi muziki na mwaka 1992 akatoa albamu ya kwanza. Alitamba zaidi akiwa na kundi la “Cool James & Black Teacher” akishirikiana na Jose Masena kutoka Kongo. Wimbo wao maarufu zaidi ulikuwa “Dr. Feelgood” ambao ulivuma sana barani Ulaya.

Baadaye alirudi Tanzania na kuwa miongoni mwa waanzilishi wa Tanzania Music Awards, akihamasisha muziki wa kizazi kipya. Nyimbo zake kama “Sina Makosa”, “Godfather”, na “Karubandika” zilipendwa sana, zikichanganya midundo ya kimataifa na ladha ya Kiswahili.

Cool James alifariki dunia kwa ajali ya gari mnamo Agosti 27, 2002, akiwa na miaka 32 tu. Pamoja na umaarufu wake, alijulikana kwa unyenyekevu, moyo wa kusaidia wasanii wachanga, na kujivunia kuwa Mtanzania.

Leo, Cool James anakumbukwa kama shujaa wa muziki wa Bongo aliyelivusha jina la Tanzania kimataifa akiwa kweli Mtoto wa Dandu.

Credit: Issa Michuzi
 
Mdau kutoka Mtandaoni aitwae Shanel Frank ni miongoni mwa Mashuhuda wa ajali ya Mtoto wa Dandu mwaka 2002

Alieleza katika ukurasa wa facebook kuwa

"Mwamba alikata upepo kwenye ajali mbaya iliyomtokea katika eneo la Millenium Tower kwenye mwaka 2002 hv.

Nakumbuka siku hiyo nilichelewa kurudi nikitokea mjini, kipindi naishi maeneo ya Sinza Mori, Kijitonyama ndanindani maarufu kama Samia Saloon.

Nilipofika pale Millenium Tower majira ya saa tano sita usiku hivi nilikuta Mistubishi Rocky, niliyokuja kufahamu baadayw kuwa ilikuwa ikiendeshwa na Mtoto wa Dandu, iligongana na Nissan Patrol (Safari) nyeupe hivi, iliyokuwa imetumbukia mtaroni, upande wa ilipokuwa Brake Point Bar na watu walikuwa busy kujaribu kuokoa maisha ya majeruhi wote kutoka katika hizo gari.

Sikuwa nikifahamu ajali iliwahusu nani na nani usiku huo, asubuhi ndipo taarifa za kifo cha Mtoto wa Dandu zikatapakaa kwenye vyombo vya habari, vikihusisha sababu ya kifo kuwa ni ile ajali niliyoiona uaiku ule.

Mwamba atakumbukwa kwa kumodernise muziki wa hapa nchini. Nakumbuka aliwahi kuishi na kufanya kazi nje ya nchi. Aliweza pia kupata colabo ya Systeme Madilu. Alikuwa ni mwanamuziki hasa.

Tutaendelea kumbukumba mwamba kwa mchango wake katika ukuzaji .

Continue to RIP Mtoto Wa Dandu."

Chini ni picha ya ushuhuda huo
Screenshot_20260319-175414~2.jpg
 
Back
Top