john achila mukumwa
Member
Nuhu aliwezaje kuwatambua wanyama wote na kuwaingiza kwenye Safina?
Biblia inatuambia kuhusu kazi aliyopewa Nuhu, ya kuviingiza katika Safina, viumbe virukavyo, vya kiume na vya kike kwa jinsi yake, na kila namna ya wanyama wa kiume na wa kike kwa jinsi yake.
Kitabu cha Mwanzo 7:
2 “Katika Wanyama wote walio safi ujitwalie saba-saba, mume na mke; na katika wanyama wasio safi wawili-wawili, mume na mke,
3 Tena katika ndege wa angani saba-saba, mume na mke; ili kuhifadhi hai mbegu juu ya uso wa nchi yote”.
Swali linakuwa, je, Nuhu alipata wapi ujuzi huo wa kuvitambua hivyo viumbe vyote, na je, hao wanyama wote aliwatolea wapi?
Ukisoma kitabu cha Mwanzo 6:20, Biblia inasema: “Katika vyote virukavyo kwa jinsi yake, na kila namna ya mnyama kwa jinsi yake, kila kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake, wawili wa kila namna WATAKUJA KWAKO ILI UWAHIFADHI”.
Unaona hilo neno “WATAKUJA KWAKO ILI UWAHIFADHI”.
Hiyo ni kuthibitisha kuwa siyo wanyama wote Nuhu alikwenda kuwachunguza kujua jinsia zao au kuwakamata, hapana. Wengine walikuja wenyewe. MUNGU MWENYEWE NDIYE ALIYEWAPELEKA kwenye Safina, isipokuwa wale wa kufugwa, ambao wao wanajulikana.
Wengi wa hao waliosalia, Mungu aliwapeleka mwenyewe kwa Nuhu.
Kazi ya Nuhu ilikuwa ni kuwaingiza tu ndani ya Safina, ambayo ilikuwa ni ya gorofa tatu.
Hiyo inaonyesha ukuu na uweza wa Mungu.
Kinachoshindina kwa binadamu, kwa Mungu hakuna kinachoshindikana.
Biblia inatuambia kuhusu kazi aliyopewa Nuhu, ya kuviingiza katika Safina, viumbe virukavyo, vya kiume na vya kike kwa jinsi yake, na kila namna ya wanyama wa kiume na wa kike kwa jinsi yake.
Kitabu cha Mwanzo 7:
2 “Katika Wanyama wote walio safi ujitwalie saba-saba, mume na mke; na katika wanyama wasio safi wawili-wawili, mume na mke,
3 Tena katika ndege wa angani saba-saba, mume na mke; ili kuhifadhi hai mbegu juu ya uso wa nchi yote”.
Swali linakuwa, je, Nuhu alipata wapi ujuzi huo wa kuvitambua hivyo viumbe vyote, na je, hao wanyama wote aliwatolea wapi?
Ukisoma kitabu cha Mwanzo 6:20, Biblia inasema: “Katika vyote virukavyo kwa jinsi yake, na kila namna ya mnyama kwa jinsi yake, kila kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake, wawili wa kila namna WATAKUJA KWAKO ILI UWAHIFADHI”.
Unaona hilo neno “WATAKUJA KWAKO ILI UWAHIFADHI”.
Hiyo ni kuthibitisha kuwa siyo wanyama wote Nuhu alikwenda kuwachunguza kujua jinsia zao au kuwakamata, hapana. Wengine walikuja wenyewe. MUNGU MWENYEWE NDIYE ALIYEWAPELEKA kwenye Safina, isipokuwa wale wa kufugwa, ambao wao wanajulikana.
Wengi wa hao waliosalia, Mungu aliwapeleka mwenyewe kwa Nuhu.
Kazi ya Nuhu ilikuwa ni kuwaingiza tu ndani ya Safina, ambayo ilikuwa ni ya gorofa tatu.
Hiyo inaonyesha ukuu na uweza wa Mungu.
Kinachoshindina kwa binadamu, kwa Mungu hakuna kinachoshindikana.