Kasomi
JT Founder
Kutana na daktari anayesaidia wagonjwa kufa badala ya kupona
Tahadhari: Ripoti hii ina maelezo ya wazi ya taratibu zinazopelekea kifo.
"Akiwa amelala kwenye varanda ya jengo la ghorofa. Ni mazingira mazuri, na marafiki wakiwa karibu naye. Ninakaribia kumdunga dawa, na anashika mikono yangu, ananitazama machoni, na kusema, 'Dkt. Green, hii kidogo itaonekana kuwa sio sawa, lakini nafkiri umeokoa maisha yangu. Asante sana.'"
"Wakati kama huo hauwezi kusahaulika," anasema daktari wa Canada Stefanie Green.
Lakini kinyume na inavyoonekana, dawa alizompa kwa njia ya mishipa na mgonjwa akitoa shukrani, hazikuwa tiba ya maumivu yasiyovumilika aliyokuwa akiyasikia.
Dawa hizo zilikuwa ni mchanganyiko wa vitu ambavyo vingemuua ndani ya dakika chache.
Stefanie Green ni miongoni mwa madaktari wa kwanza wanaosaidia watu kufa nchini Canada. Yeye pia ni mwandishi wa kitabu chake cha kumbukumbu kiitwacho "This is Assisted Dying," ambamo anasimulia uzoefu wake katika tasnia ya utabibu.
Tovuti yake inasema, kusaidiwa kufa sio kumaliza maisha ya mtu.
"Magonjwa na mateso ndio chanzo cha kugeukia chaguo hilo. Ninavyoelewa mimi, kusaidia kufa inaegemea zaidi kwenye kutimiza matakwa ya mtu."
Green ameolewa na msomi wa Kibrazili, ana watoto wawili, na anaishi Victoria, katika jimbo la Canada la British Columbia.
Nchini Canada, sheria imeruhusu kusaidiwa kufa kwa karibu miaka kumi.
Mnamo mwaka wa 2016, nchi hiyo kwanza ilianzisha sheria inayoruhusu maombi ya kusaidiwa kufa kwa watu wazima walio na magonjwa yasiyotibika ambayo husababisha mateso yasiyovumilika au wagonjwa mahututi.
Mnamo mwaka 2021, kanuni zililegezwa ili kuruhusu wagonjwa wasio na magonjwa yasiotibika ambao wanaugua sana pia kusaidiwa kufa.
Na kuna mipango ya kuwezesha kusaidia kufa watu wazima walio na magonjwa ya akili pekee, bila hali zingine, ndani ya miaka miwili.
Green, mtaalam wa suala hili na aliyejitolea kwa miaka kusaidia wagonjwa wanaotaka kufa, anaakisi jambo ambalo linaweza kuonekana kama kinzani kwa wengi: wazo la daktari kusaidia wagonjwa kufa.
Green anatumia 75% ya wakati wake kusaidia watu kufa
"Watu wengi wanafikiri jukumu letu kama madaktari ni kuokoa maisha, na kwa kiasi fulani hiyo ni kweli. Lakini nadhani kiini cha kile ambacho daktari hufanya ni kuwasaidia watu," Green anasema.
"Tunasaidia watu kupambana na magonjwa, lakini mara nyingi hatuna chochote cha kuwasaidia nacho. Tunakumbana na magonjwa ambayo hatuwezi kukabiliana nayo na kufanikiwa. Na jukumu letu si kuwatelekeza wagonjwa," anaelezea BBC News Brasil.
"Ninaamini jukumu la daktari ni kusaidia watu katika hatua zote za maisha yao, na kusaidiwa kufa ni sehemu ya hilo."
Stefanie Green ana umri wa miaka 56. Alianza maisha yake ya kitaaluma akifanya kazi kama daktari mkuu na baadaye akajitolea kutunza wanawake wajawazito, kuwasaidia wakati wanajifungua, na watoto wachanga wanapozaliwa.
Baada ya zaidi ya miongo miwili katika tasnia hiyo, mnamo mwaka 2016, wakati sheria ya Canada ilipoanza kuruhusu raia kusaidiwa kufa, Green alibadilisha mwelekeo wake wa kazi.
Leo anatumia 75% ya wakati wake kusaidia watu kufa.
Namna nilivyobadili mtazamo
Green anaeleza kwamba anaona kuna ufanano mkubwa kati ya ujuzi unaohitajika kwa madaktari na kusaidia mgonjwa kufa.
Kwake yeye, wakati wa kuzaliwa na kifo cha mtu, jukumu la daktari ni kuwa mwongozo katika mchakato wa asili.
Lakini alipoulizwa kwa nini alibadili mtazamo wake hadi kusaidia watu kufa, alitaja mambo kadhaa.
"Nilipinga sana wazo la kuacha kazi niliyokuwa nikifanya wakati nasaidia wanawake kujifungua," anasema. "Sikuweza kufikiria kitu kingine chochote ambacho kinaweza kunifurahisha kama hicho."
Hata hivyo, anasema kadiri miaka ilivyosonga, ilizidi kuwa vigumu kwake kijihisi sawa kutokana na zamu ndefu anapokuwa kazini akisaidia kina mama kujifungua.
Ilikuwa katika kipindi hiki ambapo Canada ilihalalisha kusaidia watu kufa. Green anasema alikuwa amefuatilia majadiliano kwa karibu mno.
"Kwa miaka 25 ya uzoefu wa kliniki, nimeona vifo vingi. Vifo vizuri, lakini pia vifo vibaya," anasema.
Siku chache baada ya sheria kuanza kutekelezwa, mgonjwa wa kwanza aligonga mlango wake. "Niko tayari, alisema."
Zaidi soma https://bbc.in/3F4hSrj
Chanzo BBC Swahili
Tahadhari: Ripoti hii ina maelezo ya wazi ya taratibu zinazopelekea kifo.
"Akiwa amelala kwenye varanda ya jengo la ghorofa. Ni mazingira mazuri, na marafiki wakiwa karibu naye. Ninakaribia kumdunga dawa, na anashika mikono yangu, ananitazama machoni, na kusema, 'Dkt. Green, hii kidogo itaonekana kuwa sio sawa, lakini nafkiri umeokoa maisha yangu. Asante sana.'"
"Wakati kama huo hauwezi kusahaulika," anasema daktari wa Canada Stefanie Green.
Lakini kinyume na inavyoonekana, dawa alizompa kwa njia ya mishipa na mgonjwa akitoa shukrani, hazikuwa tiba ya maumivu yasiyovumilika aliyokuwa akiyasikia.
Dawa hizo zilikuwa ni mchanganyiko wa vitu ambavyo vingemuua ndani ya dakika chache.
Stefanie Green ni miongoni mwa madaktari wa kwanza wanaosaidia watu kufa nchini Canada. Yeye pia ni mwandishi wa kitabu chake cha kumbukumbu kiitwacho "This is Assisted Dying," ambamo anasimulia uzoefu wake katika tasnia ya utabibu.
Tovuti yake inasema, kusaidiwa kufa sio kumaliza maisha ya mtu.
"Magonjwa na mateso ndio chanzo cha kugeukia chaguo hilo. Ninavyoelewa mimi, kusaidia kufa inaegemea zaidi kwenye kutimiza matakwa ya mtu."
Green ameolewa na msomi wa Kibrazili, ana watoto wawili, na anaishi Victoria, katika jimbo la Canada la British Columbia.
Nchini Canada, sheria imeruhusu kusaidiwa kufa kwa karibu miaka kumi.
Mnamo mwaka wa 2016, nchi hiyo kwanza ilianzisha sheria inayoruhusu maombi ya kusaidiwa kufa kwa watu wazima walio na magonjwa yasiyotibika ambayo husababisha mateso yasiyovumilika au wagonjwa mahututi.
Mnamo mwaka 2021, kanuni zililegezwa ili kuruhusu wagonjwa wasio na magonjwa yasiotibika ambao wanaugua sana pia kusaidiwa kufa.
Na kuna mipango ya kuwezesha kusaidia kufa watu wazima walio na magonjwa ya akili pekee, bila hali zingine, ndani ya miaka miwili.
Green, mtaalam wa suala hili na aliyejitolea kwa miaka kusaidia wagonjwa wanaotaka kufa, anaakisi jambo ambalo linaweza kuonekana kama kinzani kwa wengi: wazo la daktari kusaidia wagonjwa kufa.
Green anatumia 75% ya wakati wake kusaidia watu kufa
"Watu wengi wanafikiri jukumu letu kama madaktari ni kuokoa maisha, na kwa kiasi fulani hiyo ni kweli. Lakini nadhani kiini cha kile ambacho daktari hufanya ni kuwasaidia watu," Green anasema.
"Tunasaidia watu kupambana na magonjwa, lakini mara nyingi hatuna chochote cha kuwasaidia nacho. Tunakumbana na magonjwa ambayo hatuwezi kukabiliana nayo na kufanikiwa. Na jukumu letu si kuwatelekeza wagonjwa," anaelezea BBC News Brasil.
"Ninaamini jukumu la daktari ni kusaidia watu katika hatua zote za maisha yao, na kusaidiwa kufa ni sehemu ya hilo."
Stefanie Green ana umri wa miaka 56. Alianza maisha yake ya kitaaluma akifanya kazi kama daktari mkuu na baadaye akajitolea kutunza wanawake wajawazito, kuwasaidia wakati wanajifungua, na watoto wachanga wanapozaliwa.
Baada ya zaidi ya miongo miwili katika tasnia hiyo, mnamo mwaka 2016, wakati sheria ya Canada ilipoanza kuruhusu raia kusaidiwa kufa, Green alibadilisha mwelekeo wake wa kazi.
Leo anatumia 75% ya wakati wake kusaidia watu kufa.
Namna nilivyobadili mtazamo
Green anaeleza kwamba anaona kuna ufanano mkubwa kati ya ujuzi unaohitajika kwa madaktari na kusaidia mgonjwa kufa.
Kwake yeye, wakati wa kuzaliwa na kifo cha mtu, jukumu la daktari ni kuwa mwongozo katika mchakato wa asili.
Lakini alipoulizwa kwa nini alibadili mtazamo wake hadi kusaidia watu kufa, alitaja mambo kadhaa.
"Nilipinga sana wazo la kuacha kazi niliyokuwa nikifanya wakati nasaidia wanawake kujifungua," anasema. "Sikuweza kufikiria kitu kingine chochote ambacho kinaweza kunifurahisha kama hicho."
Hata hivyo, anasema kadiri miaka ilivyosonga, ilizidi kuwa vigumu kwake kijihisi sawa kutokana na zamu ndefu anapokuwa kazini akisaidia kina mama kujifungua.
Ilikuwa katika kipindi hiki ambapo Canada ilihalalisha kusaidia watu kufa. Green anasema alikuwa amefuatilia majadiliano kwa karibu mno.
"Kwa miaka 25 ya uzoefu wa kliniki, nimeona vifo vingi. Vifo vizuri, lakini pia vifo vibaya," anasema.
Siku chache baada ya sheria kuanza kutekelezwa, mgonjwa wa kwanza aligonga mlango wake. "Niko tayari, alisema."
Zaidi soma https://bbc.in/3F4hSrj
Chanzo BBC Swahili