Kasomi
JT Founder
Kocha mkuu wa klabu ya Manchester United, Reuben Amorim anaamini itawasaidia vyema wachezaji wake kuondoka Kuala Lumpur huku sauti za kuzomewa zikisikika masikioni mwao baada ya kufungwa 1-0 na timu ya ASEAN All-Stars.
Baada ya kukata tamaa katika kampeni kali ya Ligi Kuu ya Premier kwa ushindi dhidi ya Aston Villa siku ya Jumapili, Man United ilisafiri maili 6,600 hadi Malaysia na kukosa afueni ya matatizo yanayowakumba.
Chini ya saa 24 baaada ya mshambuliaji wa Klabu ya Wolves Matheus Cunha kuruhusiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu kabla ya kukamilisha uhamisho wa dau la £62.5m kujiunga na United, Mkosi wa mabao uliwakumba tena katika mechi ya kwanza ya ziara ya baada ya msimu uliopita barani Asia.
Wakiwa katika hali ya nyuzi joto 30 na unyevu wa juu, kikosi cha Amorim kilishindwa kutumia fursa au nafasi kadhaa walizopata licha ya mabadiliko ya wachezaji ya mara kwa mara hali iliyomaanisha kuwa waliishia kutumia wachezaji 25 wa ziada.
Bao la kipindi cha pili kutoka kwa winga wa Myanmar Maung Maung Lwin lilitosha kuipa ushindi timu hiyo ya kusini Mashariki mwa bara Asia mbele ya mashabiki 72,550 waliohudhuria katika Uwanja wa Bukit Jalil, na kuzua kuzomwa na baadhi ya mashabiki kutoka moja wakati wa filimbi ya mwisho ya mechi mbao walikuwa wamelipa hadi pauni 260 kutazama United kwenye ziara yao ya kwanza Malaysia tangu 2009.
"Siku zote ninahisi hatia kwa uchezaji wa timu yangu tangu mchezo wa kwanza nilipowasili hapa," alisema Amorim.