Kasomi
JT Founder
Mnamo mwezi wa Februari 2018, mtu mwenye silaha alivamia katika shule ya sekondari ya Marjory Stoneman Dauglasiliyopo Parkland, Florida, na kuwauwa watu 17.
Lakini badala ya kuathiriwa na tukio hilo baya, vijana wengi walionusurika na ufyatuaji huo wa risasi walianza kampeni ya kitaifa kujaribu kumaliza ghasia za bunduki.
Emma González, wakati huo akiwa na umri wa miaka18 pekee, alijitokeza kama mmoja wa viongozi wa vuguvugu hili jipya na akawa muasisi mwenza wa kikundi kilichozungumzia kuhusu haja ya udhibiti wa silaha kinachojulikana kama Vever Again MSD .
Mwezi Machi 2018, alitoa hotuba nzito katika maandamano yaliyolenga kuhimiza udhibiti wa silaha nchini Marekani - March for Our Lives mjini Washington, D.C. wakati ambapo alisoma wazi majina ya wanafunzi wenzake waliofariki na kukaa kimya kwa mud awa dakika nne- muda uliotumiwa na mshambuliaji kufanya shambulio.