Kasomi
JT Founder
Nkosi Johnson alizaliwa 1989 na kufariki dunia 2001. Nkosi alizaliwa na maambukizi ya HIV/AIDS - aliyoyarithi kutoka kwa wazazi wake. Katika mwaka 1997, alikataliwa kujiunga na shule ya umma kwasababu ya hali yake ya HIV.
Hata hivyo alikuwa mwanakampeni mkuu wa jinsi waathiriwa wa HIV wanavyopaswa kuchukuliwa sawa na watu wengine na kwa heshima katika kipindi ambacho kulikuwa na ubaguzi mkubwa dhidi ya watu wenye maambukizi hao.
Pamoja na mama yake mlezi, alianzisha kituo cha wakimbizi cha akina mama na watoto wao wenye HIV. Alipokea Tuzo ya Amani ya Watoto . Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela alimuelezea- kama ‘alama ya mapambano kwa ajili ya maisha.’
Chanzo: BBC