Advertise here

Iran yajibu shambulizi kwa jeshi la Marekani

Kasomi

JT Founder
Screenshot_20250623-232205~2.png

Iran imejibu mapigo kwa kurusha makombora katika kambi ya kijeshi ya Marekani ya Al-Udeid iliyoko nchini Qatar, ikiwa ni hatua ya kulipiza kisasi baada ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya vinu vya nyuklia vya Iran mwishoni mwa wiki.

Kituo hicho, ambacho ni miongoni mwa ngome kuu za jeshi la Marekani katika Ukanda wa Ghuba, kililengwa pamoja na kambi nyingine ya Marekani nchini Iraq.

Qatar imethibitisha kutokea kwa shambulizi hilo na imelaani vikali hatua hiyo, ikisema kuwa ni ukiukaji mkubwa wa mamlaka yake ya anga na uhuru wa taifa. Serikali ya Qatar imesema ina haki ya kujibu mapigo moja kwa moja dhidi ya mashambulizi hayo kwa mujibu wa sheria za kimataifa.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali ya Iran, Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ndilo lililoongoza mashambulizi hayo dhidi ya kambi za Marekani nchini Iraq na Qatar. Qatar imethibitisha kushambuliwa kwa kambi ya Al-Udeid, ambayo ni makao makuu ya operesheni za Marekani katika eneo la Ghuba.

Akizungumza kwa niaba ya serikali, Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya Qatar, Majed al-Ansari, alisema: "Shambulizi la IRGC kwenye kambi ya Al-Udeid ni ukiukaji wa wazi wa mamlaka ya anga ya Qatar, uhuru wetu wa kitaifa na Katiba ya Umoja wa Mataifa. Tunayo haki yetu ya kujibu moja kwa moja kwa mashambulizi haya kulingana na sheria za kimataifa."

Aliongeza kuwa mifumo ya ulinzi wa anga ya Qatar iliweza kugundua na kuharibu makombora ya Iran kabla hayajaleta madhara makubwa, na hatua za usalama zilichukuliwa haraka kulinda raia na wageni waliopo nchini humo.

Chanzo: ManaraTv
 
Back
Top