Advertise here

Bongo Zozo ajiuzulu Rasmi nafasi ya ubalozi wa utalii Tanzania kisa uvunjifu wa Amani

Kasomi

JT Founder
ANAANDIKA BONGO ZOZO "BALOZI WA UTALII TANZANIA".
1762698557456.jpg

Kutokana na hali ya uvunjifu wa amani na kupotea kwa utu nchini Tanzania, nimeamua kujiuzulu rasmi katika nafasi yangu ya Balozi wa Utalii.

Nimesikitika sana kuwaangusha Watanzania kwa ujumla, pamoja na ndugu yangu aliyeniteua, Mheshimiwa "Hamisi Kigwangalla", na marafiki wengi niliowapata kupitia jukumu hili.

Ninawashukuru kwa moyo wangu wote kwa imani, upendo, na fursa mlizonipa. Ila kwa maumivu makubwa ninayohisi moyoni, nimegundua siwezi kuendelea - siwezi, siwezi siwezi hadi siku nitakapopoa.

Namwomba Mungu siku hiyo ifike mapema, ili aondoe maumivu haya moyoni mwangu na nirejee na amani ndani yangu na katika nchi ya Tanzania.

MWISHO
 
Back
Top