Advertise here

Tunajitahidi kuboresha JamiiTalk kuwa Salama na haraka kutumia

Kasomi

JT Founder
Wana bodi ili kuifanya JT kuwa salama, rahisi kutumia na kupata mijadala kuna baadhi ya hatua tumezifanya (Tumeongeza na kuboresha).
Baadhi ya maboresho hayo ni;

1- kuwezesha hatua ya njia mbili za uthibitisho (Two-step verification)
NJia hii inafanya akaunti yako kuwa salama na kuepuka matumizi ya akaunti yako yasiyo salama. Njia hii inakuwezesha kuweka njia mbadala au kuongeza ili kuifikia Account yako, hapa unaweza tumia Email yako ili kupata code au unaweza scan code.
Screenshot_20220623-022953~2.png

Punde ukifanya hivyo utatumia msimbo wa uthibitisho.
Ku enable two step verification bonyeza Account yako kisha sehemu ya Account security, au bonyeza hapa

2- Kuweka upya nywila ulio sahau (New password reset)
Kwa sasa ukisahau password Yako hakuna haja ya kuomba msaada wa staff members Bali uta recover mwenyewe password yako.
Hivyo ili kuweza upya password yako bonyeza sehemu iliyo andikwa forgot/lost password kisha weka email yako uliyo tumia kwenye account yako, na utapewa kiungo cha kuweka upya password yako uliyo sahau.
Screenshot_20220623-023059~2.png


3- Pata Arifa (Activities summary) kwa barua pepe (email)
Kwa sasa unaweza Pata Arifa kwa barua pepe yako ikiwa mtu amekutumia ujumbe kwa PM, ametoa hisia kwenye chapisho lako au unalo fuata, au ukiwa na muda hujatembelea jukwaani.
Pia utapata Arifa ya mijadala uliyo kosa.
Vyote hivyo vitatumwa kwa email yako, hivyo inashauriwa Kutumia email iliyo active ili kupata Arifa hizo.
Screenshot_20220623-021003~2.png

Endapo kama hupati Arifa kwa barua pepe yako unaweza hakikisha kama inatumika au tembelea mipangilio ya akaunti yako sehemu ya preference kisha ruhusa kupata Arifa kwa email, au bonyeza hapa

Pia unaweza ku enable notification sehemu hiyo ili kupata taarifa hata ukiwa nje ya JamiiTalk.
 
Two-step verification
Two-step verification increases the security of your account by requiring you to provide an additional code to complete the login process. If your password is ever compromised, this verification will help prevent unauthorized access to your account.
 
Back
Top