Advertise here

TANZIA Mwanachuo wa SUA afariki kwa kujinyonga, polisi wanafanya uchunguzi

Kasomi

JT Founder
1741545346302.jpg

MOROGORO: Jeshi la Polisi limesema linachunguza tukio la kifo cha Yosia Johani Keya (25) Mwanachuo Mwaka wa Tatu katika Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) baada ya kukutwa akiwa amejinyonga kwa kutumia shuka alilofunga kwenye Kenchi la Makazi ya Wanachuo upande wa Baraza la Nyuma

Taarifa ya Polisi imeeleza tukio hilo limetokea Machi 9, 2025 asubuhi Kampasi ya Mazimbu, Kata ya Mazimbu, Manispaa ya Morogoro ambapo uchunguzi wa tukio hilo umeanza ili kubaini chanzo cha tukio hilo

Jeshi la Polisi limetoa wito Watu kutumia madawati mbalimbali ya ushauri nasaha na nasihi kueleza changamoto zao badala ya kuchukua Sheria mkononi
 
Back
Top