Advertise here

Historia ya Papa Francis kutoka Amerika ya Kusini ambaye alilibadilisha Kanisa Katoliki

Kasomi

JT Founder
Francis: Papa kutoka Amerika ya Kusini ambaye alilibadilisha Kanisa Katoliki
1049

Mwaka 2013 Francis alikuwa Papa wa kwanza kutoka Amerika na kutoka Ulimwengu wa Kusini. Alimrithi Benedict XVI, ambaye alifariki mwaka 2022. Benedict XVI alikuwa Papa wa kwanza kustaafu kwa hiari baada ya takribani miaka 600.

Papa Francis jina lake kamili ni Jorge Mario Bergoglio, alikuwa Kardinali wa Argentina, na alikuwa na umri wa miaka sabini alipokuwa Papa mwaka 2013.

Bergoglio aliwavutia wahafidhina juu ya mtazamo wake kwa masuala ya mahusiano, huku akiwavutia wanamageuzi kwa msimamo wake wa kiliberali juu ya haki za kijamii.

Lakini ndani ya urasimu wa Vatikani baadhi ya majaribio ya Francis ya kuleta mageuzi yalikumbana na upinzani, lakini alibaki kuwa maarufu miongoni mwa wanamapokeo.

Historia ya Papa Francis
Kuanzia wakati wa kuchaguliwa kwake, Francis alionyesha kuwa atafanya mambo tofauti. Aliwapokea makadinali wake kwa njia isiyo rasmi ya kusimama - badala ya kuketi kwenye kiti cha enzi cha upapa.

Tarehe 13 Machi 2013, Papa Francis alijitokeza kwenye roshani inayoangalia bustani ya St Peter's Square.

Akiwa amevalia mavazi meupe, alipewa jina jipya ambalo lilimtukuza Mtakatifu Francis wa Assisi, aliyekuwa mhubiri wa Karne ya 13 na mpenda wanyama.

Papa mpya aliweka misheni ya maadili kwa wafuasi bilioni 1.2 wa kanisa lake. "Oh, napendelea Kanisa maskini, na kwa watu maskini," alisema.

Jorge Mario Bergoglio alizaliwa huko Buenos Aires, Argentina, tarehe 17 Desemba 1936 – yeye ni mtoto mkubwa kati ya watoto watano. Wazazi wake walikimbia nchi yao ya asili ya Italia ili kuepuka maovu ya ufashisti.

Alipenda mchezo wa tango (ngoma ya asili ya Argentina) na akawa shabiki wa klabu yake ya soka ya mtaani ya, San Lorenzo.

Alipona baada ya kuugua nimonia, na kufanyiwa upasuaji wa kuondoa sehemu ya pafu lake. Na hilo lilimuacha katika hatari ya kuambukizwa katika maisha yake yote.

Akiwa mzee pia alipatwa na maumivu kwenye goti lake la kulia, ambayo aliyataja kuwa ni "unyonge wa kimwili."

Bergoglio akiwa kijana alifanya kazi kama mlinzi wa klabu ya usiku na kufanya kazi ya ufagiaji, kabla ya kuhitimu chuo kama mwanakemia.

Alifanya kazi katika kiwanda cha ndani na Esther Ballestrino, mwanaharakati aliyefanya kampeni dhidi ya udikteta wa kijeshi wa Argentina. Mwanamke huyo alitekwa, akapotea na hakupatikana tena.

Akawa Mjesuti, akasoma falsafa na kufundisha fasihi na saikolojia. Alitawazwa muongo mmoja baadaye, na kuwa mkuu wa mkoa wa kanisa hilo nchini Argentina 1973.
Screenshot_20250421-165902~2.png

Jorge Mario Bergoglio akiwa mvulana wa shule huko Buenos Aires katika miaka ya 1940
Bergoglio akiwa kijana alifanya kazi kama mlinzi wa klabu ya usiku na kufanya kazi ya ufagiaji, kabla ya kuhitimu chuo kama mwanakemia.

Alifanya kazi katika kiwanda cha ndani na Esther Ballestrino, mwanaharakati aliyefanya kampeni dhidi ya udikteta wa kijeshi wa Argentina. Mwanamke huyo alitekwa, akapotea na hakupatikana tena.

Akawa Mjesuti, akasoma falsafa na kufundisha fasihi na saikolojia. Alitawazwa muongo mmoja baadaye, na kuwa mkuu wa mkoa wa kanisa hilo nchini Argentina 1973.
 
Back
Top