Kasomi
JT Founder
Moshi mweupe umeonekana ukifuka kutoka kwenye bomba la moshi katika Kanisa la Sistine Chapel, ni wazi mchakato wa upigaji kura umekamilika na makadinali wamemchagua mrithi wa Papa Francis.
Bado hatujui ni nani amechaguliwa, lakini itaonekana wazi watakapotokea kwenye roshani ya Kanisa la Sistine, ndani ya kama saa moja.
Nini kinatokea sasa?
Makadinali wateule sasa wamemchagua Papa mpya na mambo yatakwenda kwa haraka sana kuanzia sasa.
Kwa vile moshi mweupe umetokea, kawaida, Papa mpya ataonekana kwenye roshani upande wa moja kwa moja na uwanja wa St Peter's Square ndani ya saa moja ijayo.
Papa mpya sasa anaongozwa hadi kwenye chumba kidogo karibu na Kanisa la Sistine ambapo atavaa mavazi meupe ya papa.
Kardinali mkuu hivi karibuni atathibitisha uamuzi huo kwa maneno "Habemus Papam" - Kilatini ikimaanisha "tuna Papa" - na kumtambulisha Papa mpya kwa jina lake alilochagua la papa.
Umati wajawa na furaha na kuomba wakisherehekea Papa mpya
Shangwe isiyo na kifani yashuhudiwa upande wa waumini huku moshi mweupe ukifuka, kila mtu akiwa anakimbilia kuuona.
Watu wanaruka juu na chini kwa furaha, wengine wanaomba huku wakiwa wanatazama angani. Wanandoa kutoka Ugiriki wanasema "ni tukio ambalo ni nadra sana kutokea maishani", na kuongeza kuwa watasubiri kuona Papa mpya akitokea kwenye roshani.
Katina eneo lote la Kanisa la Sistine, kengele zinalia kwa nguvu sana na zinasikika kila mahali huku watu wakishangilia na kupiga mayowe kwa furaha.
Sauti hapa ni nzuri sana, kengele zinalia kwa nguvu sana na zinasikika kila mahali huku watu wakishangilia na kupiga mayowe kwa furaha
Pia Soma
New Alert: - Kadinali Robert Prevost ndiye Papa mpya
Kadinali Robert Prevost ametangazwa kuwa Papa mpya. Robert Kardinali Prevost anatokea Chicago nchini Marekani, na hadi kuchaguliwa kwake alikuwa akihudumu kama mkuu wa Dicastery wa kanisa kwa Maaskofu. Prevost ametumia muda wake mwingi akitumikia nchini Peru, na ana uraia wa Marekani na Peru...