Kasomi
JT Founder
Mbivu na mbichi ya Profesa Janabi katika uchaguzi wa Mkurugenzi wa WHO Afrika
Uchaguzi wa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unafanyika Mei 18 huko Geneva Uswisi.
Mataifa wanachama wanapiga kura katika kikao cha pili maalum cha kamati ya kikanda ya shirika hilo, kumchagua mkurugenzi mpya wa WHO Afrika .
Mshindi anakuja kuiziba nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Kanda hiyo, Dk. Faustine Ndugulile, waziri wa wa zamani wa afya Tanzania, aliyefariki ghafla Novemba 2024.
Janabi ni mmoja wa wataalamu wakubwa wa afya nchini Tanzania, akiwa pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)
Mkurugenzi wa Kanda anachaguliwa kwa kura ya siri katika kikao cha ndani cha Kamati ya Kanda ya WHO kwa Afrika, ambayo ilikutana Januari 14, 2025, na kuamua kutumia utaratibu wa haraka, kumpata Mkurugenzi wa Kanda badala ya mchakato wa kawaida ambayo huchukua muda mrefu.
Mkurugenzi huyo anatarajiwa kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano na ana fursa ya kuchaguliwa tena upya mara moja pekee baada ya kuhudumu awamu ya kwanza.
Kwa mgombea atakayechaguliwa katika wadhifa huo, atakuwa na jukumu muhimu la kuunda sera za afya, kuratibu huduma za dharura na kushinikiza suluhu mpya za afya kote barani Afrika.
Ujumbe wa serikali ya Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Afya Jenista Mhagama, unaendeleza kampeni za kumnadi Prof Janabi, huko Uswisi.
Chanzo: BBC Swahili
Uchaguzi wa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unafanyika Mei 18 huko Geneva Uswisi.
Mataifa wanachama wanapiga kura katika kikao cha pili maalum cha kamati ya kikanda ya shirika hilo, kumchagua mkurugenzi mpya wa WHO Afrika .
Mshindi anakuja kuiziba nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Kanda hiyo, Dk. Faustine Ndugulile, waziri wa wa zamani wa afya Tanzania, aliyefariki ghafla Novemba 2024.
Janabi ni mmoja wa wataalamu wakubwa wa afya nchini Tanzania, akiwa pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)
Mkurugenzi wa Kanda anachaguliwa kwa kura ya siri katika kikao cha ndani cha Kamati ya Kanda ya WHO kwa Afrika, ambayo ilikutana Januari 14, 2025, na kuamua kutumia utaratibu wa haraka, kumpata Mkurugenzi wa Kanda badala ya mchakato wa kawaida ambayo huchukua muda mrefu.
Mkurugenzi huyo anatarajiwa kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano na ana fursa ya kuchaguliwa tena upya mara moja pekee baada ya kuhudumu awamu ya kwanza.
Kwa mgombea atakayechaguliwa katika wadhifa huo, atakuwa na jukumu muhimu la kuunda sera za afya, kuratibu huduma za dharura na kushinikiza suluhu mpya za afya kote barani Afrika.
Ujumbe wa serikali ya Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Afya Jenista Mhagama, unaendeleza kampeni za kumnadi Prof Janabi, huko Uswisi.
Chanzo: BBC Swahili