Kasomi
JT Founder
DODOMA: Mbunge wa Moshi Vijijini, Prof. Patrick Ndakidemi ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kutumia watu maarufu kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo hapa nchini.
-
Akizungumza wakati akichangia hoja kwenye makadirio ya bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii amesema kuwa ili kuongeza idadi ya watalii wana michezo maarufu kama Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Serena William watumike kupiga jeki sekta hiyo.