Kasomi
JT Founder
HISTORIA YA DR. JOHN THOBURN WILLIAMSON
John Thoburn Williamson alizaliwa huko Montfort, Quebec mnamo tarehe 10 Februari 1907, ni wapili kuzaliwa kati ya watoto wanne kwenye familia yao. Baba yake, Bertie J Williamson,alikuwa ni Mscotland ambaye alikuwa amehamia Canada kutokae Ireland. Mama yake, Rose C Boyd alikuwa Mfaransa.
Mnamo mwaka 1919 Familia hiyo ilihama kutoka Montfort na kuhamia Montreal ambapo John alienda shule ya upili ya Macdonald huko Ste Annede Bellevue. Kutoka hapo aliingia Chuo Kikuu cha Mc Gill mnamo 1925 ambapo alisoma sheria. lakini baadae
aliamua kubadili masomo na kusoma jiografia.
Alipata shahada ya BA mnamo 1928, Shahada ya Uzamili ya Sayansi mnamo 1930 na Shahada ya Uzamivu mnamo 1933. Profesa wake wa zamani wa Jiolojia, Dk Richard Graham, alialikwa Johannesburg kukagua ardhi ambayo kampuni ya De Beers walita kakufanya uchunguzi. Williamson aliongozana na Dk Graham na kutoa hotuba fupi katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand.
Baada ya hapo John T. Williamson alialikwa kujiunga na kampuni ndogo ya De Beers Consolidines Mines, kama mtaalam wa jiolojia ambapo alikubali.
Kampuni hiyo ilikuwa ikifanya utafiti wa shaba katika nchi ya Rhodesia ya kaskazini mashariki, (Zimbabwe)
Dr Williamson aliwafuata wakurungezi wa De Beers na kuwaomba wamdhamini akafanye utafiti wa madini ya almasi katika nchi ya Tanganyika lakini walimkatalia na akaamua kujiuzulu kufanya kazi katika kampuni hiyo.
Dr Williamson aliamua kujiunga na Kampuniya Tanganyika Gold and Diamond Development
mnamo1935, akifanyakazi chini ya mtaalam wao mkuu wa jiolojia, Hank Le Tendresse, Mmarekani ambaye alimkubali Sana John Thoburn Williamson, Hata hivyo hakulidhika kufanyakazi Na kampuni hiyo. Mnamo Mei 1936 Dr Williamson alisafiri kwenda Mwanza kumtafuta Wakili mwenye asili ya Asia aliyekuwa anasheshimika sana, Bw Iqbal Chand Chopra KC. Walikutana tarehe 16 Mei1936.
Bwana Iqbal anasem,"Dr John Thoburn Williamson, aliletewa ndani ya chumba cha ofisi yangu akiwa na shati nyeupe na suruali ya khaki alitaka nimsaidie mambo ya kisheria ili aweze kufanya kazi yake ya utafiti wamadini ya almasi, na alihitaji kufadhiliwa pia."
Mnamo mwaka 1937 Kampuni ya Tanganyika Goldand Diamond Development ilisitisha shughuli za utafiti na kuanzia hapo Dr Williamson akawa huru kufanya kazi peke yake. Bwana Chopra aliungana na Dr Williamson na wakaanza kazi ya utafiti wa almasi. Waliaza utafiti pembezoni mwa Ziwa Victoria na Mikoa ya Magharibi bila mafanikio yoyote.
Alivumilia huko msituni na wavulana wawili wa aminifu wa Kiafrika, Bundala na James. Dr Williamson alikuwa ameweka kambi katika kijiji cha Kizumbi (mkoa wa shinyanga) na alikuwa anazunguka huku na huko akifanya utafiti wake na kisha kurudi kambini kwake. Na hakuwa na mtaji wa kutosha ilifikia hatua akabakiwa na dolla100 tu.
Hali hiyo ilimuweka njia panda kwani vifaa vyake vilikuwa vinahitaji matengenezo na wafanyakazi wake walikiwa wanamdai mshahara. Aliamua kupunguza wafanyakazi na kuamua kumalizia mchanga wake ili afungashe vilago aondoke zake. Wakati wanamalizia kuuosha mchanga huo alipata vipande viwili vya almasi vichafu kimoja kikiwa na uzito wa kareti 30, almasi hiyo ilimpa nguvu ya kuendelea na kazi.
ITAENDELEA
Sehemu ya 1
John Thoburn Williamson alizaliwa huko Montfort, Quebec mnamo tarehe 10 Februari 1907, ni wapili kuzaliwa kati ya watoto wanne kwenye familia yao. Baba yake, Bertie J Williamson,alikuwa ni Mscotland ambaye alikuwa amehamia Canada kutokae Ireland. Mama yake, Rose C Boyd alikuwa Mfaransa.
Mnamo mwaka 1919 Familia hiyo ilihama kutoka Montfort na kuhamia Montreal ambapo John alienda shule ya upili ya Macdonald huko Ste Annede Bellevue. Kutoka hapo aliingia Chuo Kikuu cha Mc Gill mnamo 1925 ambapo alisoma sheria. lakini baadae
aliamua kubadili masomo na kusoma jiografia.
Alipata shahada ya BA mnamo 1928, Shahada ya Uzamili ya Sayansi mnamo 1930 na Shahada ya Uzamivu mnamo 1933. Profesa wake wa zamani wa Jiolojia, Dk Richard Graham, alialikwa Johannesburg kukagua ardhi ambayo kampuni ya De Beers walita kakufanya uchunguzi. Williamson aliongozana na Dk Graham na kutoa hotuba fupi katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand.
Baada ya hapo John T. Williamson alialikwa kujiunga na kampuni ndogo ya De Beers Consolidines Mines, kama mtaalam wa jiolojia ambapo alikubali.
Kampuni hiyo ilikuwa ikifanya utafiti wa shaba katika nchi ya Rhodesia ya kaskazini mashariki, (Zimbabwe)
Dr Williamson aliwafuata wakurungezi wa De Beers na kuwaomba wamdhamini akafanye utafiti wa madini ya almasi katika nchi ya Tanganyika lakini walimkatalia na akaamua kujiuzulu kufanya kazi katika kampuni hiyo.
Dr Williamson aliamua kujiunga na Kampuniya Tanganyika Gold and Diamond Development
mnamo1935, akifanyakazi chini ya mtaalam wao mkuu wa jiolojia, Hank Le Tendresse, Mmarekani ambaye alimkubali Sana John Thoburn Williamson, Hata hivyo hakulidhika kufanyakazi Na kampuni hiyo. Mnamo Mei 1936 Dr Williamson alisafiri kwenda Mwanza kumtafuta Wakili mwenye asili ya Asia aliyekuwa anasheshimika sana, Bw Iqbal Chand Chopra KC. Walikutana tarehe 16 Mei1936.
Bwana Iqbal anasem,"Dr John Thoburn Williamson, aliletewa ndani ya chumba cha ofisi yangu akiwa na shati nyeupe na suruali ya khaki alitaka nimsaidie mambo ya kisheria ili aweze kufanya kazi yake ya utafiti wamadini ya almasi, na alihitaji kufadhiliwa pia."
Mnamo mwaka 1937 Kampuni ya Tanganyika Goldand Diamond Development ilisitisha shughuli za utafiti na kuanzia hapo Dr Williamson akawa huru kufanya kazi peke yake. Bwana Chopra aliungana na Dr Williamson na wakaanza kazi ya utafiti wa almasi. Waliaza utafiti pembezoni mwa Ziwa Victoria na Mikoa ya Magharibi bila mafanikio yoyote.
Alivumilia huko msituni na wavulana wawili wa aminifu wa Kiafrika, Bundala na James. Dr Williamson alikuwa ameweka kambi katika kijiji cha Kizumbi (mkoa wa shinyanga) na alikuwa anazunguka huku na huko akifanya utafiti wake na kisha kurudi kambini kwake. Na hakuwa na mtaji wa kutosha ilifikia hatua akabakiwa na dolla100 tu.
Hali hiyo ilimuweka njia panda kwani vifaa vyake vilikuwa vinahitaji matengenezo na wafanyakazi wake walikiwa wanamdai mshahara. Aliamua kupunguza wafanyakazi na kuamua kumalizia mchanga wake ili afungashe vilago aondoke zake. Wakati wanamalizia kuuosha mchanga huo alipata vipande viwili vya almasi vichafu kimoja kikiwa na uzito wa kareti 30, almasi hiyo ilimpa nguvu ya kuendelea na kazi.
ITAENDELEA