Kasomi
JT Founder
Muungano wa wawekezaji unaoongozwa na Elon Musk ulitoa ofa ya $97.4bn kununua OpenAI, watengenezaji wa ChatGPT.
Wakili wa bilionea huyo, Marc Toberoff, alithibitisha kuwa aliwasilisha ofa ya "mali zote" za kampuni ya Musk kwa bodi yake Jumatatu.
Ofa hiyo ni mabadiliko ya hivi punde katika vita vya muda mrefu kati ya Musk, mtu tajiri zaidi duniani ambaye pia yuko karibu sana na Rais wa Marekani Donald Trump, na mkurugenzi mtendaji wa Open AI Sam Altman juu ya mustakabali wa teknolojia hii mpya ya AI inayovuma.
Akijibu ofa hiyo, Altman aliweka ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Musk wa X : akisema "hapana, asante lakini tutanunua twitter kwa $9.74 bilioni ukipenda."
OpenAI inasifiwa sana kwa kusaidia katika utengenezaji wa zana za kijasusi kwa kutumia akili mnemba na kuibua uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo.
Musk na Altman walianzisha kampuni hiyo mnamo 2015 kama kampuni isiyo ya faida, lakini uhusiano wao umezorota tangu mkuu wa Tesla na X alipojiondoa kwenye kampuni hiyo mnamo mwaka 2018.
Soma zaidi:
DeepSeek: Programu ya akili mnemba ya China kwenye rada ya usalama wa Marekani
Chat GPT4: Je, ulimwengu umejiandaa kwa dhuruba ya AI inayokuja?
Wakili wa bilionea huyo, Marc Toberoff, alithibitisha kuwa aliwasilisha ofa ya "mali zote" za kampuni ya Musk kwa bodi yake Jumatatu.
Ofa hiyo ni mabadiliko ya hivi punde katika vita vya muda mrefu kati ya Musk, mtu tajiri zaidi duniani ambaye pia yuko karibu sana na Rais wa Marekani Donald Trump, na mkurugenzi mtendaji wa Open AI Sam Altman juu ya mustakabali wa teknolojia hii mpya ya AI inayovuma.
Akijibu ofa hiyo, Altman aliweka ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Musk wa X : akisema "hapana, asante lakini tutanunua twitter kwa $9.74 bilioni ukipenda."
OpenAI inasifiwa sana kwa kusaidia katika utengenezaji wa zana za kijasusi kwa kutumia akili mnemba na kuibua uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo.
Musk na Altman walianzisha kampuni hiyo mnamo 2015 kama kampuni isiyo ya faida, lakini uhusiano wao umezorota tangu mkuu wa Tesla na X alipojiondoa kwenye kampuni hiyo mnamo mwaka 2018.
Soma zaidi:
DeepSeek: Programu ya akili mnemba ya China kwenye rada ya usalama wa Marekani
Chat GPT4: Je, ulimwengu umejiandaa kwa dhuruba ya AI inayokuja?