Advertise here

Luhaga Mpina aenguliwa kugombea Ubunge Jimbo la kisesa

Kasomi

JT Founder
1752349262928.jpg

🟢 Safari ya Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, ndani ya Bunge kupitia CCM huenda ikafikia ukingoni mwaka huu

Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina, ametupwa nje ya mbio za kuwania tena ubunge kupitia CCM mwaka huu! 🛑

Taarifa kutoka vikao vya chama ngazi ya wilaya ya Meatu na mkoa wa Simiyu zinasema jina la Mpina halikupendekezwa kuendelea na mchakato wa uteuzi. Hii ni baada ya kamati ya siasa ya CCM kumwondoa kwenye orodha ya wagombea.

Mpina, ambaye amejulikana kwa miaka ya hivi karibuni kwa msimamo wake mkali na kuibana serikali Bungeni, sasa amewekwa pembeni.

Majina matatu Waliopitishwa kwenda hatua ya juu ya mchakato ni:
âś… Sitta Risinge
âś… Mussa Mbuga
âś… Silinde Gumada

Hata hivyo, bado kuna nafasi ya mwisho, kwani Kamati Kuu ya CCM Taifa inaweza kuamua kurudisha jina lolote iliyoona linafaa—ikiwemo la Mpina.

Credit: Halisimax
 
Back
Top