Advertise here

Mwanaume aamka na kukuta meli kubwa kwenye bustani yake

Kasomi

JT Founder
Mwanaume amka na kukuta meli kubwa kwenye bustani yake
1748010823953.jpg

Je, Meli hii ilifikaje kwenye nyumba yake?

Mwanaume mmoja huko Norway aliamka na kukuta meli kubwa ya kubebea mizigo ikiwa imetia nanga kwenye bustani yake.

Meli hiyo yenye urefu wa mita 135 (443ft) nusra igonge nyumba ya Johan Helberg siku ya Alhamisi.

Bw Helberg alifahamishwa kuhusu tukio hilo na jirani yake aliyejawa na hofu ambaye alikuwa ameona meli hiyo ilipokuwa ikielekea moja kwa moja ufukweni upande wa nyumba yake, huko Byneset, karibu na Trondheim.

"Kengele ya mlango ililia wakati wa mchana ambapo sipendi kufungua," Bw Helberg aliambia kituo cha televisheni cha TV2.

"Nilienda dirishani na nikashangaa sana kuona meli kubwa," alisema katika mahojiano na Guardian.

"Ilinibidi niinamishe shingo yangu ili kuona sehemu ya juu. Sikuamini."

"Mita tano zaidi upande wa kusini ingeingia chumbani," aliongeza wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji la Norway. "Sikusikia chochote."

Jirani Jostein Jorgensen alisema aliamshwa na mlio wa meli hiyo ilipokuwa ikielekea nchi kavu kwa kasi, na kukimbilia nyumbani kwa Bw Helberg.

"Nilikuwa na uhakika kwamba tayari alikuwa ameshatoka kwa sababu hakukuwa na dalili ya mtu kuwa ndani. Niligonga kengele ya mlango mara nyingi bila kusikia chochote," alisema Bw Jorgensen.

“Na hapo ndipo nilipompigia simu na kuwasiliana naye,” aliiambia TV2.

Hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo.

Haijulikani ni nini kilisababisha ajali hiyo na polisi wa Norway wanasemekana wanafanya uchunguzi.

Chanzo: BBC Swahili, TV2
 
Back
Top