Advertise here

Hii ndiyo orodha ya wabunge walioingoza Kishapu kuanzia 1965 - 2025

Kasomi

JT Founder
JIMBO LA KISHAPU

Leo tuangalie historia ya jimbo la Kishapu upande wa Wabunge, Bunge la kwanza la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania 1965 mkoa wa Shinyanga uliwakilishwa na Majimbo matatu (3) amabayo ni Shinyanga Mashariki, (kwa sasa ndiyo kishapu) Shinyanga Kati na Shinyanga Magharibi.

BUNGE LA KWANZA.
Mbunge wa kwanza wa jimbo la Shinyanga Mashariki ni;

Mhe. Edward Elikana Bukumba Nzingula

Shinyanga Mashariki (TANU)

Kuanzia 12 Okt. 1965 -30 Juni, 1969.

Akafatia Mhe. Maganga Masanja Shija II (TANU)

Kuanzia 16 Dis. 1969 -24 Julai, 1970.

BUNGE LA PILI.
Uchaguzi wa mwaka 1970 Jimbo la Shinyanga Mashariki likabadilishwa jina likaitwa jimbo la Mwadui na aliyeshinda ubunge ni;

Mhe. Edward Elikana Bukumba Nzingula

Mwadui (TANU)

Kuanzia 19 Nov. 1970 –18 Julai, 1975

BUNGE LA TATU.
Uchaguzi wa mwaka 1975 jimbo la Mwadui likabadilishwa jina tena na kuitwa jimbo la Shinyanga Vijijini na aliyeshinda uchaguzi ni;

Mhe Edward Elikana Bukumba Nzingula

Shinyanga Vijijini (TANU/ CCM)

Kuanzia 06 Nov. 1975 –1979

Mhe. Henry Mnyashi Limihagati (CCM)

Kuanzia 06 Jan. 1980 –26 Julai, 1980

BUNGE LA NNE.
Uchaguzi wa 1980 jimbo la Shinyanga Vijijini likabakia na jina lilelile na mbunge ni;

Mhe. Henry Mnyashi Limihagati

Shinyanga Vijijini (CCM)

Kuanzia 04 Nov. 1980 –31 Julai, 1985

BUNGE LA TANO.
Uchaguzi wa mwaka 1985 jimbo la Shinyanga Vijijini likagawanywa na kuwa na majimbo mawili Solwa na Kishapu. Mbunge wa kwanza wa jimbo la Kishapu ni;

Mhe. Paulo Ng’wala Makolo

Kishapu (CCM)
Kuanzia 02 Nov. 1985 -23 Julai, 1990

BUNGE LA SITA.
Uchaguzi wa mwaka 1990 jimbo la Kishapu mbunge wake akabaki ni yule yule,

Mhe. Paulo Ng’wala Makolo

Kishapu (CCM)
Kuanzia 06 Nov. 1990 –04 Agosti, 1995

BUNGE LA SABA.
Uchaguzi wa mwaka 1995 Mbunge wa jimbo la Kishapu akabaki yule yule,

Mhe. Paul Ngwala Makolo

Kishapu (CCM)
Kuanzia 24 Nov. 1995 -04 Agosti, 2000

BUNGE LA NANE.
Uchaguzi wa mwaka 2000 jimbo la Kishapu mbunge akabaki yule yule,

Mhe. Paul Ng’wala Makolo

Kishapu (CCM)
Kuanzia 14 Nov. 2000 -05 Agosti, 2005

BUNGE LA TISA.
Uchaguzi wa mwaka 2005 jimbo la Kishapu likapata mbunge mpya ambaye ni;

Mhe. Fred Tungu Mpendazoe

Kishapu (CCM)
Kuanzia 28 Dis. 2005 -01 Agosti, 2010

BUNGE LA KUMI.
Uchaguzi wa mwaka 2010 jimbo la Kishapu likapata mbunge mpya tena ambaye ni;

Mhe. Suleiman Masoud Nchambi Suleiman

Kishapu (CCM)
Kuanzia 12 Nov. 2010 –7 Agosti, 2015

BUNGE LA KUMI NA MOJA.
Uchaguzi wa mwaka 2015 jimbo la Kishapu mbunge wake akabiki yule yule,

Mhe. Suleiman Masoud Nchambi

Kishapu (CCM)
Kuanzia 17 Nov. 2015 -31 Julai, 2020

BUNGE LA KUMI NA MBILI.
Uchaguzi wa mwaka 2020 jimbo la Kishapu likapata mbunge mpya tena ambaye ni;

Mhe. Boniphace Nyangindu Butondo

Kishapu (CCM)
Kuanzia 6 Nov. 2020-13 Julai. 2025

BUNGE LA KUMI NA TATU.
Uchaguzi wa mwaka 2025 jimbo la Kishapu likapata mbunge mpya tena ambaye ni;

Mhe. Lucy Thomas Mayenga

Kishapu (CCM)
Kuanzia 11 Nov. 2025 hadi sasa.

Hii ndiyo orodha ya wabunge walioingoza Kishapu yetu mpaka sasa, je kwenye hii orodha ni wabunge wangapi ambao umewashuhudia. Mimi nimeanzia kwa Paul Makolo.

Imeandikwa na Faida Potea Mjukuu wa Njelekela mwana wa kunyumba mpenda kumbukumbu
 
Back
Top