Simulizi
Member
Simulizi: GENERAL’S DAUGHTER (01)
Mtunzi: Kalmas Konzo
Simu: 0625 646265
Camp 26 ilikuwa ni kambi maalum ambayo ilikuwa imeandaliwa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa kikosi maalum ambacho kilikuwa kimekusudiwa kuanzishwa na jeshi la ulinzi la Bantu. Kazi ya kikosi hiki itakuwa ni kutekeleza misheni mbalimbali za usalama wa Taifa pindi zitakapokuwa zimeandaliwa. Kikosi hiki kilipewa ina la THE 5 EAGLES’ SQUAD.
Askari mbalimbali wa jeshi walikusanywa kutoka katika vikosi mbalimbali vya jeshi nchi Bantu na kuletwa katika kambi hii. Lengo lilikuwa ni kupatiwa mafunzo yenye mitihani mizito sana. Kutoka katika askari jeshi hao walitakiwa askari watano tu ambao wangekuwa wamefuzu na kuunda kikosi cha THE 5 EAGLE’S SQUAD
Miongoni mwa askari jeshi waliokuwa wakitarajiwa kupata mafunzo katika kambi hii maalum, mimi nilikuwa ni mmoja wao.
Jina langu ni Wilson Julius. Mimi ni askari jeshi kutoka katika Jeshi la ulinzi kikosi namba mbili kilichopo jijini Kano. Mimi ni askari mahiri sana katika utendaji wangu wa kazi. Sifa hii ndiyo ilifanya niwe miongoni mwa wachaguliwa wa kupata mafunzo katika kambi ile maalum ya kijeshi ambayo ilikuwa imeanzsihwa.
Camp 26 ilikuwa ni kambi ambayo ilikuwa ikipatikana katikati ya nchi ya Bantu kilometa sabini kutoka mini. Eneo ambako ilikuwepo kambi hii lilikuwa ni eneo la misitu pasi na makazi ya watu. Hakukuwa na usafiri maalum wa kuweza kukufikisha huko.
Yalikuwa ni majira ya saa tisa za alasiri ndipo nilipowasili katika kambi hii. Nilikuwa nimechoka sana kwani nilikuwa nimetumia usafiri wa punda kwa sababu magari hayakuruhusiwa kuja katika eneo la kambi.
Kambi hii ilikuwa ni ya kuvutia sana. Ilikuwa na majengo mbalimbali ya ghorofa ambayo yalikuwa ya kisasa sana. Nadhani majengo haya baadhi ni ofisi, madarasa pamoja na mabweni. Kambi hii ilikuwa imeandaliwa kwa muda mrefu kwani ilikuwa na miundo mbinu yote muhimu. Inaonekana serikali ilikuwa imewekeza fedha za kutosha katika mradi huu.
Niliibeba mizigo yang una moja kwa moja niliekea mpaka getini mahali maalum kwa ajili ya mapokezi. Pale getini palikuwa na askari watatu ambao walikuwa na silaha nzito kabisa.
“Jambo afande! Naitwa Wilson Julius, mwanafunzi katika kambi hii!” niliongea nikitoa kitambulisho changu na kumkabidhi mmoja wa askari wale.
Askari yule hakujibu chochote zaidi ya kukipokea kitambulisho changu na kuanza kukikagua.
Alitumia kama dakika moja na nusu kukikagua kitambulisho kile. Baada ya hapo aliuinua uso wake na kunitazama akijaribu kulinganusha picha iliyokuwepo kwenye kitambulisho na sura yangu.
Nilishangaa ni kwa nini askari huyu alikuwa akichukua muda mrefu sana katika kukikagua kitambulisho. Lakini baadaye nilijipa jibu kwamba ile ilikuwa ni kazi yake na alikuwa akionyesha umakini katika kazi.
Baada ya kujiridhisha, aliinua simu na kisha akapiga. Sikuelewa alikuwa akipiga wapi na alikuwa akiongea nini kwani nilichosikia ni "Sawa" na kisha simu ikakatwa.
Baada ya kama dakika tano hivi nilipigwa na butwaa kubwa sana. Ndani ya uzio kutoka katika jengo mojawapo macho yangu yaliweza kumwona mwanamke mkoja akija pale getini.
Mwanamke huyu alikuwa mzuri sana. Alikuwa na kila sifa ya uzuri wa mwanamke ambayo wewe ulikuwa ukiifahamu. Alikuwa amejaaliwa kila kitu kuanzia uzuri wa sura, rangi mpaka umbile.
Katika maisha yangu sikuwa nimewahi kumwona mwanamke mzuri kama yule yule.
"Hivi hapa nipo kambi ya jeshi kweli?" nilijiuliza moyoni pasi kuwa na jibu.
"Kijana vipi?" askari mmoja aliniulshtua kwa kuniuliza mara baada ya kuona nimezama katika lindi la duwao huku macho yangu nikiwa nimeyatoa kuelekea kwa mrembo yule.
"Ah! Hapana afande!" nilijibu huku nikizuga kuonyesha kwamba nilikuwa katika hali ya kawaida.
Jambo jingine lililonishangaza kuliko yote ilikuwa ni pindi alipofika pale getini. Mwanamke yule mrembo katika sare yake ya jeshi iliyomkaa vema alikuwa amechafukwa na nyota za kutosha. Nilipochunguza zaidi niligundua kwamba alikuwa na cheo cha Major General.
Askari wote pale getini walipiga saluti za heshima kwa mkubwa wao. Nami niliungana nao kwa kuiangusha saluti moja matata ya kikakamavu.
"Pole kwa safari afande!" askari yule aliniambia kwa sauti nyororo na ya upole yenye kuweza kumtoa nyoka pangoni.
"Ahsante sana!" nilijibu huku nikiwa nimeduwaa.
Alinitazama kwa muda wa sekunde kadhaa mithili ya mtu aliyekuwa akinifananisha. Kitendo kile kilinifanya nijishtukie na kujihisi huenda labda nilikuwa na kasoro fulani.
"Nifuate!" askari yule mrembo aliongea na kuanza kuondoka.
Niliibeba mizigo yangu na kuanza kumfuata. Jambo ambalo lilinishangaza ni kwamba iweje askari mwenye cheo kikubwa kama yule ndo aje kunipokea! Nilibaki kuogelea katika bahari ya swali like pasi kuwa na jibu.
Safari ya kumfuata ikiendelea.
Jambo la kushangaza ni kwamba mwanamke yule alinichukua mpaka katika uwanja wa mazoezi. Sikujua alikuwa na lengo gani kwani kwa fikra zangu mimi nilidhani labda ningechukuliwa mpaka katika hosteli ambako ningeoga na baadaye ningepewa chakula.
Hakika ilibaki kuwa ajabu kwangu.
"Weka mizigo chini!" mwanamke yule aliongea kwa sauti yake ile ile ya upole yenye mvuto.
Niliweka mizigo chini na kusimama kwa ukakamavu mbele yake kwani askari yule alikuwa amenizidi cheo mbali sana.
"Unaitwa nani?" niliulizwa.
"Naitwa Wilson Julius afande!" nilijibu kwa ujasiri.
"Sasa hivi ni saa ngapi?" aliniuliza.
"Ni saa tisa alasiri afande!" nilijibu kwa ukakamavu macho yakiwa mbele.
"Muda wa mwisho kuripoti uliambiwa ni saa ngapi?" aliuliza tena.
Kwa swali lile hapo ndipo akili yangu ikaanza kunikaa sawa. Nikajua tayari mambo yalikuwa yamekwishaharibika.
"Saa sita mchana afande!" nilijibu.
"Sasa ni kwa nini umefika saa hizi? Mbaya zaidi leo ndiyo siku ya mwisho kuripoti. Au unafikiri hili ni jeshi la baba yako!" niliulizwa.
ENDELEA
Mtunzi: Kalmas Konzo
Simu: 0625 646265
Camp 26 ilikuwa ni kambi maalum ambayo ilikuwa imeandaliwa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa kikosi maalum ambacho kilikuwa kimekusudiwa kuanzishwa na jeshi la ulinzi la Bantu. Kazi ya kikosi hiki itakuwa ni kutekeleza misheni mbalimbali za usalama wa Taifa pindi zitakapokuwa zimeandaliwa. Kikosi hiki kilipewa ina la THE 5 EAGLES’ SQUAD.
Askari mbalimbali wa jeshi walikusanywa kutoka katika vikosi mbalimbali vya jeshi nchi Bantu na kuletwa katika kambi hii. Lengo lilikuwa ni kupatiwa mafunzo yenye mitihani mizito sana. Kutoka katika askari jeshi hao walitakiwa askari watano tu ambao wangekuwa wamefuzu na kuunda kikosi cha THE 5 EAGLE’S SQUAD
Miongoni mwa askari jeshi waliokuwa wakitarajiwa kupata mafunzo katika kambi hii maalum, mimi nilikuwa ni mmoja wao.
Jina langu ni Wilson Julius. Mimi ni askari jeshi kutoka katika Jeshi la ulinzi kikosi namba mbili kilichopo jijini Kano. Mimi ni askari mahiri sana katika utendaji wangu wa kazi. Sifa hii ndiyo ilifanya niwe miongoni mwa wachaguliwa wa kupata mafunzo katika kambi ile maalum ya kijeshi ambayo ilikuwa imeanzsihwa.
Camp 26 ilikuwa ni kambi ambayo ilikuwa ikipatikana katikati ya nchi ya Bantu kilometa sabini kutoka mini. Eneo ambako ilikuwepo kambi hii lilikuwa ni eneo la misitu pasi na makazi ya watu. Hakukuwa na usafiri maalum wa kuweza kukufikisha huko.
Yalikuwa ni majira ya saa tisa za alasiri ndipo nilipowasili katika kambi hii. Nilikuwa nimechoka sana kwani nilikuwa nimetumia usafiri wa punda kwa sababu magari hayakuruhusiwa kuja katika eneo la kambi.
Kambi hii ilikuwa ni ya kuvutia sana. Ilikuwa na majengo mbalimbali ya ghorofa ambayo yalikuwa ya kisasa sana. Nadhani majengo haya baadhi ni ofisi, madarasa pamoja na mabweni. Kambi hii ilikuwa imeandaliwa kwa muda mrefu kwani ilikuwa na miundo mbinu yote muhimu. Inaonekana serikali ilikuwa imewekeza fedha za kutosha katika mradi huu.
Niliibeba mizigo yang una moja kwa moja niliekea mpaka getini mahali maalum kwa ajili ya mapokezi. Pale getini palikuwa na askari watatu ambao walikuwa na silaha nzito kabisa.
“Jambo afande! Naitwa Wilson Julius, mwanafunzi katika kambi hii!” niliongea nikitoa kitambulisho changu na kumkabidhi mmoja wa askari wale.
Askari yule hakujibu chochote zaidi ya kukipokea kitambulisho changu na kuanza kukikagua.
Alitumia kama dakika moja na nusu kukikagua kitambulisho kile. Baada ya hapo aliuinua uso wake na kunitazama akijaribu kulinganusha picha iliyokuwepo kwenye kitambulisho na sura yangu.
Nilishangaa ni kwa nini askari huyu alikuwa akichukua muda mrefu sana katika kukikagua kitambulisho. Lakini baadaye nilijipa jibu kwamba ile ilikuwa ni kazi yake na alikuwa akionyesha umakini katika kazi.
Baada ya kujiridhisha, aliinua simu na kisha akapiga. Sikuelewa alikuwa akipiga wapi na alikuwa akiongea nini kwani nilichosikia ni "Sawa" na kisha simu ikakatwa.
Baada ya kama dakika tano hivi nilipigwa na butwaa kubwa sana. Ndani ya uzio kutoka katika jengo mojawapo macho yangu yaliweza kumwona mwanamke mkoja akija pale getini.
Mwanamke huyu alikuwa mzuri sana. Alikuwa na kila sifa ya uzuri wa mwanamke ambayo wewe ulikuwa ukiifahamu. Alikuwa amejaaliwa kila kitu kuanzia uzuri wa sura, rangi mpaka umbile.
Katika maisha yangu sikuwa nimewahi kumwona mwanamke mzuri kama yule yule.
"Hivi hapa nipo kambi ya jeshi kweli?" nilijiuliza moyoni pasi kuwa na jibu.
"Kijana vipi?" askari mmoja aliniulshtua kwa kuniuliza mara baada ya kuona nimezama katika lindi la duwao huku macho yangu nikiwa nimeyatoa kuelekea kwa mrembo yule.
"Ah! Hapana afande!" nilijibu huku nikizuga kuonyesha kwamba nilikuwa katika hali ya kawaida.
Jambo jingine lililonishangaza kuliko yote ilikuwa ni pindi alipofika pale getini. Mwanamke yule mrembo katika sare yake ya jeshi iliyomkaa vema alikuwa amechafukwa na nyota za kutosha. Nilipochunguza zaidi niligundua kwamba alikuwa na cheo cha Major General.
Askari wote pale getini walipiga saluti za heshima kwa mkubwa wao. Nami niliungana nao kwa kuiangusha saluti moja matata ya kikakamavu.
"Pole kwa safari afande!" askari yule aliniambia kwa sauti nyororo na ya upole yenye kuweza kumtoa nyoka pangoni.
"Ahsante sana!" nilijibu huku nikiwa nimeduwaa.
Alinitazama kwa muda wa sekunde kadhaa mithili ya mtu aliyekuwa akinifananisha. Kitendo kile kilinifanya nijishtukie na kujihisi huenda labda nilikuwa na kasoro fulani.
"Nifuate!" askari yule mrembo aliongea na kuanza kuondoka.
Niliibeba mizigo yangu na kuanza kumfuata. Jambo ambalo lilinishangaza ni kwamba iweje askari mwenye cheo kikubwa kama yule ndo aje kunipokea! Nilibaki kuogelea katika bahari ya swali like pasi kuwa na jibu.
Safari ya kumfuata ikiendelea.
Jambo la kushangaza ni kwamba mwanamke yule alinichukua mpaka katika uwanja wa mazoezi. Sikujua alikuwa na lengo gani kwani kwa fikra zangu mimi nilidhani labda ningechukuliwa mpaka katika hosteli ambako ningeoga na baadaye ningepewa chakula.
Hakika ilibaki kuwa ajabu kwangu.
"Weka mizigo chini!" mwanamke yule aliongea kwa sauti yake ile ile ya upole yenye mvuto.
Niliweka mizigo chini na kusimama kwa ukakamavu mbele yake kwani askari yule alikuwa amenizidi cheo mbali sana.
"Unaitwa nani?" niliulizwa.
"Naitwa Wilson Julius afande!" nilijibu kwa ujasiri.
"Sasa hivi ni saa ngapi?" aliniuliza.
"Ni saa tisa alasiri afande!" nilijibu kwa ukakamavu macho yakiwa mbele.
"Muda wa mwisho kuripoti uliambiwa ni saa ngapi?" aliuliza tena.
Kwa swali lile hapo ndipo akili yangu ikaanza kunikaa sawa. Nikajua tayari mambo yalikuwa yamekwishaharibika.
"Saa sita mchana afande!" nilijibu.
"Sasa ni kwa nini umefika saa hizi? Mbaya zaidi leo ndiyo siku ya mwisho kuripoti. Au unafikiri hili ni jeshi la baba yako!" niliulizwa.
ENDELEA