Simulizi
Member
MOYO WA KWELI
1-5
01
(Baada ya kukutana na Ava, alisahau kama safari ya mapenzi ni udanganyifu mtupu....
)
Karibu
Si kila mtu unayekutana naye katika maisha ni mdanganyifu, wengine ni faraja ilioletwa duniani kuwa tabasamu kwa watu wengine. Ni wachache sana wanaoamini katika huu kweli.
Asilimia kubwa ya watu wanaamini katika mapenzi kuna udanganyifu wa hali ya juu na si ukweli, Easton ni miongoni mwa wanaume wanaoungana na asilimia kubwa ya watu wengine kudai katika mapenzi kuna udanganyifu.
"Watu watakuheshimu zaidi endapo utauthibitishia ulimwengu kuwa upo kwenye mahusiano, mtangaze mpenzi wako siku ya kesho....niamini Mimi hata maadui zako watakuheshimu" Secretary Jo alizungumza kwa ushawishi
"Sivutiwi na mahusiano kwa sasa.... kitendo nilichomtendea Sophia bado kina jirudia kichwani mwangu ingawa ni miaka 7 sasa imepita" Easton (CEO wa Kampuni ya Penfolds inayojihusisha na utengenezaji wa wine aina ya Shiraz) alizungumza
"Sitaki kusikia kuhusu miaka 7 iliyopita, kuna uvumi umezagaa kuwa huenda wewe ni shoga au rungu lako halisimami" Secretary Jo aliongea kwa sauti ya chini
"Ni wazi kabisa hata wao hawana uhakika na mashaka yao.... wachukulie hatua wote unaosikia wakiniita Mimi shoga, kama utawakalia kimya basi watahisi wewe ndio mwanamke wangu" Easton aliongea
"Vipi kuhusu rungu lako ni kweli halina nguvu?" Secretary Jo aliuliza
Easton alifungua zipu ya suruali yake, mashine ilikuwa imesimama kiasi kwamba Secretary Jo alifumba macho
"Sitaki kusikia uvumi wa aina yoyote ile....naamini kila kitu umejionea" Easton aliongea huku akifunga zipu ya suruali.
Ukweli ni kwamba Secretary Jo ana chukizwa na namna boss wake anavyokaa pekee yake kwa muda mrefu bila mahusiano. Na hii ndio sababu ameamua kutunga maneno ya uongo apate faraja ya moyo
Shughuli za hapa na pale ziliendelea katika Kampuni ya Penfolds, Easton alipita huku na kule kukagua namna wafanyakazi wake wanavyotenda kazi
"Nadhani tunahitaji kuajiri wafanyakazi wapatao 200, Kampuni letu limekuwa kwa kasi. Ina mlazimu mtu mmoja kufanya kazi za watu kumi ili kufikia malengo....na hii ndio sababu inayopelekea watu kuja wamechelewa kazini" Secretary Jo alitoa ripoti
"Andaa tangazo la kuajiri wafanyakazi wapya....pia tengeneze ratiba itakayowapa nafasi wafanyakazi kupumzika tukiwa tunasubiria wafanyakazi wapya" Easton alimuachia maagizo Secretary Jo kisha akaingia ndani ya gari lake
Alielekea Supermarket kuchukua vitu muhimu kwa ajili ya Mama yake.
Hakutumia muda mrefu kwa sababu alikuwa anajua ni kipi anaenda kuchukua.
Wakati wa kurudi ilimlazimu kukwepa barabara kuu kuepuka msongamano wa magari hivyo aliamua kupita barabara ya mtaani iliyopo pakana na makazi ya watu.
Akiwa bize anafatilia ripoti mbalimbali kupitia simu kutoka kwa wafanyakazi wake alilazamika kufunga breki ya gari baada ya kunusurika kumgonga binti mdogo aliyekuwa amelewa
Alitaka kumpotezea lakini vurugu za binti mlevi zilimlazimu kushuka kwenye gari
"Wee paka unapata wapi ujasiri wa kumsogelea Mbwa....ulikuwa salama ndani ya gari sielewi ni nini kimekutuma ushuke" Ava aliongea huku akimgonga gonga kifuani Easton na chupa
"Paka?.... umeniita paka!" Easton aliuliza
"Wewe ni paka, tena paka mweusi aliyezeeka.... haya niambie ni kitu gani utanifanya, dunia nzima inaniogopa kwa nguvu nilizojariwa, kuua na kuzika ni swala la kawaida kwangu" Ava alifoka huku machozi yakimtoka
Easton aliachia tabasamu, hakuona sababu ya kuhangaika na mlevi anayetokwa machozi. Alirudi ndani ya gari....ile anataka kuondoa gari, Ava aligonga chupa yake kwa nguvu zote kioo cha gari kikapasuka
Moyo wa Easton ulishtuka, kama asingefumba macho basi vipande vya chupa vingeingia machoni kwake
Ava ndio kushtuka kuwa ameharibu kioo cha gari la watu.
Easton alitaka kuchukua hatua lakini muonekano wa Ava ulitosha kumueleza kama atampeleka Polisi basi atafia gerezani.
Kwa hasira aliondoa gari lake akaelekea nyumbani.
Selena (Mama Easton) baada ya kuliona gari la kijana wake katika hali ile alishika mdomo wake.
Hakutaka kufikiria mara mbili alishika simu akampigia Pacco (Baba mdogo wa Easton)
"Ifike mahala umuache mwanangu apumue.....hakuna kitu utapata kwa kumchanganya na matukio ya hovyo kila siku. Naomba usisahau kama yeye ndio CEO wa Kampuni ya Penfolds.....kura za washirika ndio zimemuweka hapo alipo kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi, endapo utaendelea kumfatilia nitachukua hatua" Selena alizungumza kisha akakata simu hakutaka kusikia upande wa pili unasemaje
"Mlevi alipasua kioo cha gari na chupa yake na si Pacco" Easton alizungumza kwa ufupi
Selena aliziba mdomo wake na mkono baada ya kujua amekurupuka
Siku iliyofuatia, Ava alikuwa wa kwanza kuamka....alipita pita mtandaoni ndipo akafanikiwa kukutana na tangazo la kazi kutoka Penfolds
"Wafanyakazi kazi 200?....kwa wakati huu nitaenda kwa mganga sipo tayari kukosa nafasi pale....ndoto yangu ni kunywa wine ya Shiraz, hapana si kunywa tu nataka niwe miongoni mwa watu nitakao husika kutengeneza...." Ava alijisemea huku akipiga miayo, alikuwa na njaa kali sana
Wakati anashuka kitandani aone nini Mama yake kamuandalia alikumbuka tendo alilolifanyia gari la Easton
*02*
"Halikuwa lengo kupasua kioo cha gari lake...." Ava aliongea pekee yake akaelekea jikoni
"Huoni aibu kuamka saa tano asubuhi, nikupe pole kwa sababu hakutakuwa na chai siku ya leo" Jessica aliongea
"Nimekuja tusalimiane na si kutafuta chai" Ava aliongea
"Kabla hujanywa pombe hakikisha una akiba ya pesa vinginevyo utashikwa vidonda vya tumbo...." Jessica aliongea akijitahidi kuficha maandazi
"Nimeona tangazo la kazi mtandaoni kutoka Penfolds, watu wanao hitaji ni 200 natamani niwe miongoni mwao" Ava aliongea
"Safari hii unahitaji msaada wangu, bila kuoga maji ya baharini hautaambulia chochote....kabla hujatuma maombi ni lazima tufanye kitu," Jessica aliongea
"Kwahiyo unataka nifuate maji baharini? nitaonekana kichaa mbele za watu" Ava aliongea huku pua zake zikinusa maandazi
"Nitakusindikiza ukaoge ndani ya bahari pindi jua litakapo zama, inaweza kuwa hatari lakini faida yake ni kubwa" Jessica aliongea
"Hukuwa na haja ya kuficha maandazi, weka kwenye sahani tule wote.... tofauti na hapo sitakuwa na nguvu ya kuongea na wewe" Ava aliongea
Kwa pamoja walicheka, wawili hawa wanapendana sana
"Naamini Elon (Kaka yake Ava) huko aliko atakuwa sawa....siamini mwanangu kama alikufa ni swala la muda tu kila kitu kitarudi kwenye hali yake" Jessica alijipa natumaini
"Huna haja ya kukaa una mtaja mara kwa mara.....sijisikii kulia asubuhi hii" Ava aliongea huku machozi yakimlenga.
Walianza kula maandazi kwa pamoja wakaachana na habari ya Elon
Upande wa Easton akiwa na Secretary Jo walielekea katika Kampuni la BMW AG kununua gari lingine
"Nipe muda nimtafute mtu aliye husika kuharibu gari lako...." Secretary Jo aliongea kwa sauti ya kujipendekeza
"Yule ni panya mdogo kama ni kijaribu kutengeneza mtego nimnase nitaonekana kichaa, ni kajitu kadogo wala usisumbue akili yako, aliharibu kioo cha gari tu si vingine....kama utalihitaji ruksa kutumia" Easton aliongea
Secretary Jo aliachia tabasamu pana usoni mwake, akiwa kafumba macho alijikuta akiona idadi kubwa ya wanawake wakimshobokea kisa gari
"Nyie siyo hadhi yangu ondokeni...." Secretary Jo aliongea kwa sauti akiwa katika kufikiria
"Nina dakika 30 za kuwa hapa acha kufikiria upuuzi" Easton aliongea baada ya kugundua fikira za huyu kiumbe zipo mbali
Secretary Jo ndio kushtuka, kwa pamoja walianza kukagua gari zilizokuwa zinauzwa
Baada ya jua kuzama, Ava pamoja na Mama yake walielekea baharini.
"Hii ni bahari kuu ya Mini, kwa muonekano inatisha lakini kama utaoga maji yake matatizo yako yote yataondoka...." Jessica aliongea huku ndani ya moyo wake akiwa na uoga
"Ni kweli bahari hii inatisha....kama nitaogopa sitaweza kufanikiwa, naomba ugeukie upande mwingine sitaki unione namna navyooga" Ava aliongea
Baada ya kukubaliana alivua nguo zake kisha akaanza kusogea tararibu....ujasiri wa kukamilisha tambiko lake ulimvaa. Alijikuta akioga bila uoga...wakati anaosha miguu yake aliona mkufu, tamaa ya kuuchukua ilimuingia.
"Mkufu? una uhakika huu mkufu ulikuwa usawa wa miguu yako" Jessica alimuuliza binti yake huku akiukagua
Ava alitikisa kichwa kuashiria ndiyo
"Kamwe usije kuutupa wala kuugeuza bidhaa ya kuuza, hii ni ishara tosha kuwa tambiko lako limejibiwa.....Malkia wa bahari hii kakupa mkufu kama zawadi" Jessica aliongea huku machozi yakimlenga
Mida ya usiku Ava akiwa kavaa mkufu shingoni, alianza kutuma maombi ya kazi kupitia email iliyokuwa imewekwa kwenye tangazo.
Upande wa Easton akiwa chumbani kwake ana kunywa wine, aliikumbuka siku aliyomnyonga Mpenzi wake (Sophia) mpaka kufa.
Vitu vyote vizuri alivyowahi kumpatia alivitupa baharini ikiwemo mkufu aliokota Ava.
Katika zawadi zote alizompatia Sophia, mkufu ndio ulikuwa na gharama kubwa kuliko hata magari japo kwa muonekano ni wa kawaida sana.
"Sikuwahi kufikiria kama ulikuwa mdanganyifu.... sitamani kukumbuka kuhusu wewe, nachukia pale napo kukumbuka" Easton alizungumza huku akikunja ngumi
Ndani ya moyo wake hajawahi na hana kama atakuja kujutia kumuua Mpenzi wake.
Kulivyo pambazuka asubuhi, Ava aliingia mtandaoni. Moyo wake ulilipuka baada ya kukutana na ujumbe wa kuitwa kwenye usahili
Alipiga kelele za furaha kabla hata hajapata kazi, Mama yake aliingia bila hodi kujua kitu gani kinaendelea.
Alifumba macho yake baada ya kumfuma binti yake akiwa uchi na mwenye msitu wa kutosha
*03*
"Unawezaje kupata usingizi na hilo pori!....sikuwahi kufikiria kama wewe ni mchafu namna hii" Jessica aliongea huku akilaani kwanini ameingia bila hodi
"Hili pori ni mali yangu kwanini ukasirike!...nimeitwa kwenye usahili, kesho saa mbili asubuhi nitakuwa katika geti la Kampuni la Penfolds. Kuliko ufikirie nawezaje kuishi na hili pori, fikiria ni nguo gani nitavaa" Ava aliongea akiwa kajifunika blanket mwili mzima, ni wazi alikuwa anaona aibu
"Huna haja ya kuchanganyikiwa kuhusu mavazi, vaa kawaida ili usiwe kivutio au kituko cha kila mtu kukutazama, kama Elon angekuepo nadhani angeamua uvae nini....japo ni wa kiume lakini alikuwa bora sana kwenye swala la mavazi" Jessica aliongea kisha akaondoka
Ava alijitoa ndani ya blanket, alirudia kuutazama ujumbe uliotumwa kwenye email yake kutoka Penfolds
"Nimechoka kukaa muda mrefu bila kazi, naamini nitafanya vizuri siku ya kesho" Ava aliongea pekee yake
Upande wa Easton akiwa ofisini kwake alipitia orodha ya majina ya watu walioitwa kwenye usahili
"Katarina yupo mapokezi anahitaji kuonana na wewe.... usijaribu kumpuuzia kwa sababu figo yake inaishi ndani ya tumbo lako" Secretary Jo aliongea
"Familia yangu ilikuwa na uwezo wa kununua figo kwa gharama yoyote ile, ni ujinga wake wa kutaka kuonekana anajali sana kuhusu Mimi hivyo naomba usisumbue akili yangu mwambie nipo bize" Easton aliongea akiendelea kupitia orodha ya majina
Secretary Jo alibakia kukodoa macho, hakutarajia kama boss wake anaweza kuwa na roho ngumu namna hii
"Ni kama tumezoeana sana, kila nikitoa amri zangu hushtuki badala yake unaanza kunipangia nini nifanye....nitatafuta Secretary mwingine" Easton aliongea
"Ni...ni... samehe" Secretary Jo aliongea akarudi mapokezi kurudisha majibu
"Easton yupo bize sana lakini kaahidi kukutembelea nyumbani kwako atakapo punguza foleni ya mafaili" Secretary Jo aliongea kwa kutabasamu
"Huna haja ya kuongea uongo kwa ajili yake, ni miaka 10 imepita sasa lakini bado hajabadilika.... ahsante kwa kurudisha majibu" Katarina alizungumza kisha akaondoka
Kama si Elon (Kaka yake Ava) kumshika basi angedondoka kwenye ngazi kutokana na mawazo
"Umefanikiwa kuonana naye?" Elon aliuliza
"Easton niliyemuacha miaka 10 iliyopita hajabadilika....." Katarina aliongea huku machozi yakimlenga lenga
"Naelewa namna unavyojisikia, lakini ningefurahi kama ungeacha kumpa umuhimu mkubwa katika maisha yako.... kuna watu wengi sana wanatamani kuwa na wewe, tafadhali sana fungua moyo kwa ajili yao" Elon aliongea
"Ili Mimi na wewe tuendelee kuwa boss na mfanyakazi wake, naomba uache kuongea kitu chochote kuhusu huyo Mwanaume, pengine ulikuwa hujui lakini yeye ndio sababu ya Mimi kutafuta pesa kwa nguvu, ili niwe na msaada kwake ni lazima niwe na pesa" Katarina aliongea kisha akaingia kwenye gari
Elon hakuwa na namna aliingia kwenye gari pia, mapenzi yake kwa mwanamke huyu ni makubwa sana kiasi kwamba hakujali kukaa mbali na familia yake kwa miaka 10
Upande wa Ava akiwa chumbani kwake alimwaga nguo zake zote sakafuni lakini hakuona nguo inayomfaa kuvaa siku ya kesho.
Aliachana na nguo akaelekea kwenye kabati la viatu, moyo wake ulishtuka baada ya kila kiatu alichokuwa anagusa kukuta kina meno ya panya, bahati nzuri au mbaya alifanikiwa kumkuta panya akiwa ndani ya kiatu alichokuwa ana kiamini kuliko vyote.
Kwa hasira alizokuwa nazo alimng'ata kichwa chote akakitema sakafuni.
Jessica aliingia bila hodi tena macho yake yalitua sakafuni moja kwa moja.... alijikuta akipiga kelele hakutarajia kama binti yake anaweza kuwa na roho ngumu namna hii
"Nitafuata ushauri wako, siku ya kesho ni sawa na siku nyingine sina haja ya kuhangaika" Ava aliongea akiwa kakata tamaa
"Elon alikuwa na suti nzuri pamoja na viatu vizuri.....hakuna ubaya kama utavaa nguo zake" Jessica alimuambia binti yake kisha akaondoka
Upande wa Selena (Mama yake Easton) alifurahi ndani ya moyo wake baada ya kumuona Katarina
"Nisamehe kwa kuja nyumbani kwako bila taarifa" Katarina aliongea
"Na kumbuka mara ya mwisho nilikuambia hapa ni sawa na nyumbani kwako....nafurahi kuhusu mafanikio yako, nitajitahidi kuunga mkono ndoto zako kadiri ya uwezo wangu, niambie ni kitu gani hicho unataka nami nitakutimizia" Selena aliongea
Katarina alipiga magoti bila kujali uwepo wa Elon
"Nampenda kijana wako, naomba unisaidie niwe mke wake.... sihitaji moyo wake, kitu pekee nachohitaji Mimi ni kuhakikisha yupo salama" Katarina aliongea
Selena alijiziba mdomo wake na mkono, hakujua aseme nini, alimnyanyua magotini Katarina kwa kisingizio cha baridi
Siku iliyofuatia, Ava alivaa suti ya Elon (Kaka yake) viatu vyote vilikuwa vikubwa kwake. Hakutaka kupata taabu aliweka karatasi kwa mbele ili mguu wake ukae vizuri.
Baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa alivaa cheni ya marehemu (Sophia) aliyoiokota baharini kisha akaondoka.
Alifika katika malango ya Kampuni la Penfolds, alitaja namba yake ya usahili baada ya Walinzi kujiridhisha walimpa kitambulisho akaingia ndani.
Alijiamini kupita maelezo....alikaa kwenye kiti kisha akakunja nne
"Elon...." Kijana mmoja aliyekuwa karibu yake alimuita
Ava ndio kushtuka koti la alilovaa limeandikwa jina la Kaka yake.
"Hakuwa na haja ya kuandika majina nguo zake" Ava alijisemea kisha akajiweka bize, hakuwa tayari kuzungumza chochote na Mwanaume huyu
Akiwa hapa ametulia alimuona Elon kwa mbali akiwa kabeba pochi ya Katarina. Alifumba na kufumbua lakini hakumuona tena....aliamini wenge ndio lina msumbua lakini ukweli ni kwamba macho yake yalikuwa sahihi
Tangazo lilitolewa watu wote wasimame kwa ajili ya kumkaribisha CEO wa Kampuni ya Penfolds.
Macho ya Ava yalishtuka baada ya kumuona Easton akiwa na jopo la watu waliovaa suti kali pamoja na vitambulisho shingoni mwao
*04*
"Nimefurahi kuona nyie wote hapa mpo kwa nia ya kufanya kazi na Mimi.... huenda wengi wenu mkawa hamnifahamu, naitwa Easton ni CEO wa hili Kampuni" Easton aliongea kisha akaachia tabasamu
"Laiti ningejua huyu panya ndio CEO wa hili Kampuni nisingeji sumbua kutuma maombi" Ava aliongea pekee yake akionekana kukata tamaa
"Easton si mtu wa kuendeshwa na migogoro binafsi....sijui ni kitu gani umemkosea lakini usivunjike moyo kwa sababu hatakukumbusha kosa lako" Binti aliyekuwa amekaa jirani yake alimsaidia kumtoa hofu
"Kosa nililofanya ni la jinai, siwezi kuamini katika matumaini yako" Ava aliongea
"Kitu pekee ambacho hawezi kusamehe ni udanganyifu tena katika mapenzi....kuwa na amani" Binti huyu alizungumza....ni wazi kabisa kabla ya kuja kwenye usahili alifatilia sifa za Mwajiri wake
Ava alikaa kwa kutulia baada ya Binti huyu kumpa matumaini.
Baada ya watu wote kupata chai, usahili ulianza.
Asilimia kubwa ya watu waliamini katika uwezo wao, tofauti na Ava aliamini katika tambiko alilofanya pamoja na mkufu aliovaa.
Hatimaye aliitwa katika chumba cha usahili.
Moyo wake ulilipuka zaidi baada ya kukutana macho na Easton.
Yule Binti alikuwa sahihi, Easton alionesha dalili zote za kutomfahamu Ava.
"Nahitaji kusikia ni kitu gani utafanya kuhusu Kampuni letu pindi utakapopata nafasi" Easton aliuliza
"Nitafanya vitu vilivyo nje ya uwezo wangu" Ava alijibu
Watu wote walimshangaa kwa jibu lake, Easton alimpa ishara aelezee maana ya jibu lake
"Nitahakikisha nafanya maamuzi magumu kuliokoa Kampuni endapo litakuwa katika wakati mgumu..." Ava aliongea
Secretary Jo alimruhusu aondoke, ni wazi hakufurahishwa na majibu yake hivyo aliweka alama x kwenye jina la Ava.
Baada ya usahili kumalizika, Secretary Jo aliwasogelea wasahili wote
"Nipo hapa kwa niaba ya CEO, tunashukuru kwa ushirikiano wenu mzuri, leo saa sita kamili usiku kila mtu aingie kwenye email yake kuona matokeo ya alichofanya, kuanzia sasa na kuendelea naomba msipige simu wala kuja ofisini kuulizia majibu kwani kila kitu kitamalizika kwenye email" Secretary Jo aliongea kisha akaondoka
Mapigo ya moyo wa Ava yalikuwa juu sana, ni wazi hakuwa na uhakika na kitu alichokifanya.... alijikuta akivua koti la Kaka yake baada ya kuhisi joto. Akiwa anatembea taratibu macho yake yalitua kwenye kioo kilichokuwa ukutani....alijicheka mwenyewe kwa namna alivyoonekana kituko kwa mavazi aliyovaa.
Upande wa Penfolds alianza kupitia majina ya watu walionekana kufanya vizuri....alimtazama kwa macho makubwa Secretary Jo baada ya jina la Ava kuonekana limewekwa mkasi
"Namkumbuka huyu binti vizuri, nguo alizokuwa amevaa pamoja na viatu vinatosha kumuonesha hana nidhamu..... muonekano wake ni mbaya, kitu kingine kilicho muangusha ni aina ya jibu alilotoa, ni kama anatamaa ya kuwa CEO na si Mfanyakazi" Secretary Jo aliongea
"Kwa upande wangu anafaa, ni watu wachache sana wanaweza kufikiria kufanya maamuzi magumu kuhusu Kampuni ambalo si lake, na kuhusu muonekano hivyo ndivyo alivyo watu wengi wamekuja na mionekano bandia lakini yeye kajikubali alivyo, hivyo nampitisha.... hakikisha siku ya kesho anafika hapa ofisini kuanza kazi" Easton aliongea
Secretary Jo alitaka kupinga lakini macho ya Easton yalimnyamazisha.
Ava hakwenda nyumbani badala yake alielekea ufukweni mwa bahari kuu ya Mini, alitandika koti lake akajilaza. Kichwa chake kilikuwa tupu, hakuwa na kitu cha kufikiria zaidi ya kufumba macho.
Baada ya kuchoka kukaa mahali hapa aliondoka akasahau koti
"Koti la Elon...." Ava aliongea pekee yake baada ya kukumbuka
Alirudi ufukweni kwa kukimbia, bahati nzuri au mbaya aliparamiana na Elon (Kaka yake)
"Elon?..." Ava aliita kwa sauti ya uoga asiamini anachokiona
"Umenifananisha pole kwa hilo" Elon aliongea kisha akaondoka
Hakuwa tayari kurudi kwa familia yake sababu ya Katarina, hakuwa tayari kujua watu hawa kwa sasa wanaishije bila yeye kwa sababu ndio alikuwa mhimili mkubwa.
Ava hakutaka kuelewa, alimkimbilia Kaka yake kisha akakagua alama iliyokuwa kwenye mkono.
Machozi yalimdondoka baada ya kugundua mtu huyu ni Kaka yake wa damu kabisa
"Sitakuuliza wala kukuomba urudi nyumbani, nitajifanya sijaona chochote" Ava aliongea kisha akaondoka, hakutaka kufatilia kuhusu mkoti tena
Alifika nyumbani akiwa amelowa machozi, Jessica alimkumbatia binti yake akiwa mwenye hofu
"Elon anaishi...kwa haraka tu ana maisha mazuri, kuanzia sasa na kuendelea acha kumfikiria wala kuumia moyo kisa yeye" Ava aliongea akizidisha kulia
Jessica alikaa kimya hakujua ni maneno gani anapaswa kuongea.
Upande Easton baada ya kurejea nyumbani, aliachia tabasamu kutokana na chakula kilichokuwa mezani.
Hakusubiria kukaribishwa, alikaa akaanza kula
"Tabasamu lako usoni linatosha kuniambia Katarina ni Mpishi vizuri" Selena aliongea
Easton alidondosha kijiko, tabasamu lilipotea usoni mwake
"Kuanzia sasa nitakuwa na kula hotelini.
1-5
01
(Baada ya kukutana na Ava, alisahau kama safari ya mapenzi ni udanganyifu mtupu....
Karibu
Si kila mtu unayekutana naye katika maisha ni mdanganyifu, wengine ni faraja ilioletwa duniani kuwa tabasamu kwa watu wengine. Ni wachache sana wanaoamini katika huu kweli.
Asilimia kubwa ya watu wanaamini katika mapenzi kuna udanganyifu wa hali ya juu na si ukweli, Easton ni miongoni mwa wanaume wanaoungana na asilimia kubwa ya watu wengine kudai katika mapenzi kuna udanganyifu.
"Watu watakuheshimu zaidi endapo utauthibitishia ulimwengu kuwa upo kwenye mahusiano, mtangaze mpenzi wako siku ya kesho....niamini Mimi hata maadui zako watakuheshimu" Secretary Jo alizungumza kwa ushawishi
"Sivutiwi na mahusiano kwa sasa.... kitendo nilichomtendea Sophia bado kina jirudia kichwani mwangu ingawa ni miaka 7 sasa imepita" Easton (CEO wa Kampuni ya Penfolds inayojihusisha na utengenezaji wa wine aina ya Shiraz) alizungumza
"Sitaki kusikia kuhusu miaka 7 iliyopita, kuna uvumi umezagaa kuwa huenda wewe ni shoga au rungu lako halisimami" Secretary Jo aliongea kwa sauti ya chini
"Ni wazi kabisa hata wao hawana uhakika na mashaka yao.... wachukulie hatua wote unaosikia wakiniita Mimi shoga, kama utawakalia kimya basi watahisi wewe ndio mwanamke wangu" Easton aliongea
"Vipi kuhusu rungu lako ni kweli halina nguvu?" Secretary Jo aliuliza
Easton alifungua zipu ya suruali yake, mashine ilikuwa imesimama kiasi kwamba Secretary Jo alifumba macho
"Sitaki kusikia uvumi wa aina yoyote ile....naamini kila kitu umejionea" Easton aliongea huku akifunga zipu ya suruali.
Ukweli ni kwamba Secretary Jo ana chukizwa na namna boss wake anavyokaa pekee yake kwa muda mrefu bila mahusiano. Na hii ndio sababu ameamua kutunga maneno ya uongo apate faraja ya moyo
Shughuli za hapa na pale ziliendelea katika Kampuni ya Penfolds, Easton alipita huku na kule kukagua namna wafanyakazi wake wanavyotenda kazi
"Nadhani tunahitaji kuajiri wafanyakazi wapatao 200, Kampuni letu limekuwa kwa kasi. Ina mlazimu mtu mmoja kufanya kazi za watu kumi ili kufikia malengo....na hii ndio sababu inayopelekea watu kuja wamechelewa kazini" Secretary Jo alitoa ripoti
"Andaa tangazo la kuajiri wafanyakazi wapya....pia tengeneze ratiba itakayowapa nafasi wafanyakazi kupumzika tukiwa tunasubiria wafanyakazi wapya" Easton alimuachia maagizo Secretary Jo kisha akaingia ndani ya gari lake
Alielekea Supermarket kuchukua vitu muhimu kwa ajili ya Mama yake.
Hakutumia muda mrefu kwa sababu alikuwa anajua ni kipi anaenda kuchukua.
Wakati wa kurudi ilimlazimu kukwepa barabara kuu kuepuka msongamano wa magari hivyo aliamua kupita barabara ya mtaani iliyopo pakana na makazi ya watu.
Akiwa bize anafatilia ripoti mbalimbali kupitia simu kutoka kwa wafanyakazi wake alilazamika kufunga breki ya gari baada ya kunusurika kumgonga binti mdogo aliyekuwa amelewa
Alitaka kumpotezea lakini vurugu za binti mlevi zilimlazimu kushuka kwenye gari
"Wee paka unapata wapi ujasiri wa kumsogelea Mbwa....ulikuwa salama ndani ya gari sielewi ni nini kimekutuma ushuke" Ava aliongea huku akimgonga gonga kifuani Easton na chupa
"Paka?.... umeniita paka!" Easton aliuliza
"Wewe ni paka, tena paka mweusi aliyezeeka.... haya niambie ni kitu gani utanifanya, dunia nzima inaniogopa kwa nguvu nilizojariwa, kuua na kuzika ni swala la kawaida kwangu" Ava alifoka huku machozi yakimtoka
Easton aliachia tabasamu, hakuona sababu ya kuhangaika na mlevi anayetokwa machozi. Alirudi ndani ya gari....ile anataka kuondoa gari, Ava aligonga chupa yake kwa nguvu zote kioo cha gari kikapasuka
Moyo wa Easton ulishtuka, kama asingefumba macho basi vipande vya chupa vingeingia machoni kwake
Ava ndio kushtuka kuwa ameharibu kioo cha gari la watu.
Easton alitaka kuchukua hatua lakini muonekano wa Ava ulitosha kumueleza kama atampeleka Polisi basi atafia gerezani.
Kwa hasira aliondoa gari lake akaelekea nyumbani.
Selena (Mama Easton) baada ya kuliona gari la kijana wake katika hali ile alishika mdomo wake.
Hakutaka kufikiria mara mbili alishika simu akampigia Pacco (Baba mdogo wa Easton)
"Ifike mahala umuache mwanangu apumue.....hakuna kitu utapata kwa kumchanganya na matukio ya hovyo kila siku. Naomba usisahau kama yeye ndio CEO wa Kampuni ya Penfolds.....kura za washirika ndio zimemuweka hapo alipo kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi, endapo utaendelea kumfatilia nitachukua hatua" Selena alizungumza kisha akakata simu hakutaka kusikia upande wa pili unasemaje
"Mlevi alipasua kioo cha gari na chupa yake na si Pacco" Easton alizungumza kwa ufupi
Selena aliziba mdomo wake na mkono baada ya kujua amekurupuka
Siku iliyofuatia, Ava alikuwa wa kwanza kuamka....alipita pita mtandaoni ndipo akafanikiwa kukutana na tangazo la kazi kutoka Penfolds
"Wafanyakazi kazi 200?....kwa wakati huu nitaenda kwa mganga sipo tayari kukosa nafasi pale....ndoto yangu ni kunywa wine ya Shiraz, hapana si kunywa tu nataka niwe miongoni mwa watu nitakao husika kutengeneza...." Ava alijisemea huku akipiga miayo, alikuwa na njaa kali sana
Wakati anashuka kitandani aone nini Mama yake kamuandalia alikumbuka tendo alilolifanyia gari la Easton
*02*
"Halikuwa lengo kupasua kioo cha gari lake...." Ava aliongea pekee yake akaelekea jikoni
"Huoni aibu kuamka saa tano asubuhi, nikupe pole kwa sababu hakutakuwa na chai siku ya leo" Jessica aliongea
"Nimekuja tusalimiane na si kutafuta chai" Ava aliongea
"Kabla hujanywa pombe hakikisha una akiba ya pesa vinginevyo utashikwa vidonda vya tumbo...." Jessica aliongea akijitahidi kuficha maandazi
"Nimeona tangazo la kazi mtandaoni kutoka Penfolds, watu wanao hitaji ni 200 natamani niwe miongoni mwao" Ava aliongea
"Safari hii unahitaji msaada wangu, bila kuoga maji ya baharini hautaambulia chochote....kabla hujatuma maombi ni lazima tufanye kitu," Jessica aliongea
"Kwahiyo unataka nifuate maji baharini? nitaonekana kichaa mbele za watu" Ava aliongea huku pua zake zikinusa maandazi
"Nitakusindikiza ukaoge ndani ya bahari pindi jua litakapo zama, inaweza kuwa hatari lakini faida yake ni kubwa" Jessica aliongea
"Hukuwa na haja ya kuficha maandazi, weka kwenye sahani tule wote.... tofauti na hapo sitakuwa na nguvu ya kuongea na wewe" Ava aliongea
Kwa pamoja walicheka, wawili hawa wanapendana sana
"Naamini Elon (Kaka yake Ava) huko aliko atakuwa sawa....siamini mwanangu kama alikufa ni swala la muda tu kila kitu kitarudi kwenye hali yake" Jessica alijipa natumaini
"Huna haja ya kukaa una mtaja mara kwa mara.....sijisikii kulia asubuhi hii" Ava aliongea huku machozi yakimlenga.
Walianza kula maandazi kwa pamoja wakaachana na habari ya Elon
Upande wa Easton akiwa na Secretary Jo walielekea katika Kampuni la BMW AG kununua gari lingine
"Nipe muda nimtafute mtu aliye husika kuharibu gari lako...." Secretary Jo aliongea kwa sauti ya kujipendekeza
"Yule ni panya mdogo kama ni kijaribu kutengeneza mtego nimnase nitaonekana kichaa, ni kajitu kadogo wala usisumbue akili yako, aliharibu kioo cha gari tu si vingine....kama utalihitaji ruksa kutumia" Easton aliongea
Secretary Jo aliachia tabasamu pana usoni mwake, akiwa kafumba macho alijikuta akiona idadi kubwa ya wanawake wakimshobokea kisa gari
"Nyie siyo hadhi yangu ondokeni...." Secretary Jo aliongea kwa sauti akiwa katika kufikiria
"Nina dakika 30 za kuwa hapa acha kufikiria upuuzi" Easton aliongea baada ya kugundua fikira za huyu kiumbe zipo mbali
Secretary Jo ndio kushtuka, kwa pamoja walianza kukagua gari zilizokuwa zinauzwa
Baada ya jua kuzama, Ava pamoja na Mama yake walielekea baharini.
"Hii ni bahari kuu ya Mini, kwa muonekano inatisha lakini kama utaoga maji yake matatizo yako yote yataondoka...." Jessica aliongea huku ndani ya moyo wake akiwa na uoga
"Ni kweli bahari hii inatisha....kama nitaogopa sitaweza kufanikiwa, naomba ugeukie upande mwingine sitaki unione namna navyooga" Ava aliongea
Baada ya kukubaliana alivua nguo zake kisha akaanza kusogea tararibu....ujasiri wa kukamilisha tambiko lake ulimvaa. Alijikuta akioga bila uoga...wakati anaosha miguu yake aliona mkufu, tamaa ya kuuchukua ilimuingia.
"Mkufu? una uhakika huu mkufu ulikuwa usawa wa miguu yako" Jessica alimuuliza binti yake huku akiukagua
Ava alitikisa kichwa kuashiria ndiyo
"Kamwe usije kuutupa wala kuugeuza bidhaa ya kuuza, hii ni ishara tosha kuwa tambiko lako limejibiwa.....Malkia wa bahari hii kakupa mkufu kama zawadi" Jessica aliongea huku machozi yakimlenga
Mida ya usiku Ava akiwa kavaa mkufu shingoni, alianza kutuma maombi ya kazi kupitia email iliyokuwa imewekwa kwenye tangazo.
Upande wa Easton akiwa chumbani kwake ana kunywa wine, aliikumbuka siku aliyomnyonga Mpenzi wake (Sophia) mpaka kufa.
Vitu vyote vizuri alivyowahi kumpatia alivitupa baharini ikiwemo mkufu aliokota Ava.
Katika zawadi zote alizompatia Sophia, mkufu ndio ulikuwa na gharama kubwa kuliko hata magari japo kwa muonekano ni wa kawaida sana.
"Sikuwahi kufikiria kama ulikuwa mdanganyifu.... sitamani kukumbuka kuhusu wewe, nachukia pale napo kukumbuka" Easton alizungumza huku akikunja ngumi
Ndani ya moyo wake hajawahi na hana kama atakuja kujutia kumuua Mpenzi wake.
Kulivyo pambazuka asubuhi, Ava aliingia mtandaoni. Moyo wake ulilipuka baada ya kukutana na ujumbe wa kuitwa kwenye usahili
Alipiga kelele za furaha kabla hata hajapata kazi, Mama yake aliingia bila hodi kujua kitu gani kinaendelea.
Alifumba macho yake baada ya kumfuma binti yake akiwa uchi na mwenye msitu wa kutosha
*03*
"Unawezaje kupata usingizi na hilo pori!....sikuwahi kufikiria kama wewe ni mchafu namna hii" Jessica aliongea huku akilaani kwanini ameingia bila hodi
"Hili pori ni mali yangu kwanini ukasirike!...nimeitwa kwenye usahili, kesho saa mbili asubuhi nitakuwa katika geti la Kampuni la Penfolds. Kuliko ufikirie nawezaje kuishi na hili pori, fikiria ni nguo gani nitavaa" Ava aliongea akiwa kajifunika blanket mwili mzima, ni wazi alikuwa anaona aibu
"Huna haja ya kuchanganyikiwa kuhusu mavazi, vaa kawaida ili usiwe kivutio au kituko cha kila mtu kukutazama, kama Elon angekuepo nadhani angeamua uvae nini....japo ni wa kiume lakini alikuwa bora sana kwenye swala la mavazi" Jessica aliongea kisha akaondoka
Ava alijitoa ndani ya blanket, alirudia kuutazama ujumbe uliotumwa kwenye email yake kutoka Penfolds
"Nimechoka kukaa muda mrefu bila kazi, naamini nitafanya vizuri siku ya kesho" Ava aliongea pekee yake
Upande wa Easton akiwa ofisini kwake alipitia orodha ya majina ya watu walioitwa kwenye usahili
"Katarina yupo mapokezi anahitaji kuonana na wewe.... usijaribu kumpuuzia kwa sababu figo yake inaishi ndani ya tumbo lako" Secretary Jo aliongea
"Familia yangu ilikuwa na uwezo wa kununua figo kwa gharama yoyote ile, ni ujinga wake wa kutaka kuonekana anajali sana kuhusu Mimi hivyo naomba usisumbue akili yangu mwambie nipo bize" Easton aliongea akiendelea kupitia orodha ya majina
Secretary Jo alibakia kukodoa macho, hakutarajia kama boss wake anaweza kuwa na roho ngumu namna hii
"Ni kama tumezoeana sana, kila nikitoa amri zangu hushtuki badala yake unaanza kunipangia nini nifanye....nitatafuta Secretary mwingine" Easton aliongea
"Ni...ni... samehe" Secretary Jo aliongea akarudi mapokezi kurudisha majibu
"Easton yupo bize sana lakini kaahidi kukutembelea nyumbani kwako atakapo punguza foleni ya mafaili" Secretary Jo aliongea kwa kutabasamu
"Huna haja ya kuongea uongo kwa ajili yake, ni miaka 10 imepita sasa lakini bado hajabadilika.... ahsante kwa kurudisha majibu" Katarina alizungumza kisha akaondoka
Kama si Elon (Kaka yake Ava) kumshika basi angedondoka kwenye ngazi kutokana na mawazo
"Umefanikiwa kuonana naye?" Elon aliuliza
"Easton niliyemuacha miaka 10 iliyopita hajabadilika....." Katarina aliongea huku machozi yakimlenga lenga
"Naelewa namna unavyojisikia, lakini ningefurahi kama ungeacha kumpa umuhimu mkubwa katika maisha yako.... kuna watu wengi sana wanatamani kuwa na wewe, tafadhali sana fungua moyo kwa ajili yao" Elon aliongea
"Ili Mimi na wewe tuendelee kuwa boss na mfanyakazi wake, naomba uache kuongea kitu chochote kuhusu huyo Mwanaume, pengine ulikuwa hujui lakini yeye ndio sababu ya Mimi kutafuta pesa kwa nguvu, ili niwe na msaada kwake ni lazima niwe na pesa" Katarina aliongea kisha akaingia kwenye gari
Elon hakuwa na namna aliingia kwenye gari pia, mapenzi yake kwa mwanamke huyu ni makubwa sana kiasi kwamba hakujali kukaa mbali na familia yake kwa miaka 10
Upande wa Ava akiwa chumbani kwake alimwaga nguo zake zote sakafuni lakini hakuona nguo inayomfaa kuvaa siku ya kesho.
Aliachana na nguo akaelekea kwenye kabati la viatu, moyo wake ulishtuka baada ya kila kiatu alichokuwa anagusa kukuta kina meno ya panya, bahati nzuri au mbaya alifanikiwa kumkuta panya akiwa ndani ya kiatu alichokuwa ana kiamini kuliko vyote.
Kwa hasira alizokuwa nazo alimng'ata kichwa chote akakitema sakafuni.
Jessica aliingia bila hodi tena macho yake yalitua sakafuni moja kwa moja.... alijikuta akipiga kelele hakutarajia kama binti yake anaweza kuwa na roho ngumu namna hii
"Nitafuata ushauri wako, siku ya kesho ni sawa na siku nyingine sina haja ya kuhangaika" Ava aliongea akiwa kakata tamaa
"Elon alikuwa na suti nzuri pamoja na viatu vizuri.....hakuna ubaya kama utavaa nguo zake" Jessica alimuambia binti yake kisha akaondoka
Upande wa Selena (Mama yake Easton) alifurahi ndani ya moyo wake baada ya kumuona Katarina
"Nisamehe kwa kuja nyumbani kwako bila taarifa" Katarina aliongea
"Na kumbuka mara ya mwisho nilikuambia hapa ni sawa na nyumbani kwako....nafurahi kuhusu mafanikio yako, nitajitahidi kuunga mkono ndoto zako kadiri ya uwezo wangu, niambie ni kitu gani hicho unataka nami nitakutimizia" Selena aliongea
Katarina alipiga magoti bila kujali uwepo wa Elon
"Nampenda kijana wako, naomba unisaidie niwe mke wake.... sihitaji moyo wake, kitu pekee nachohitaji Mimi ni kuhakikisha yupo salama" Katarina aliongea
Selena alijiziba mdomo wake na mkono, hakujua aseme nini, alimnyanyua magotini Katarina kwa kisingizio cha baridi
Siku iliyofuatia, Ava alivaa suti ya Elon (Kaka yake) viatu vyote vilikuwa vikubwa kwake. Hakutaka kupata taabu aliweka karatasi kwa mbele ili mguu wake ukae vizuri.
Baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa alivaa cheni ya marehemu (Sophia) aliyoiokota baharini kisha akaondoka.
Alifika katika malango ya Kampuni la Penfolds, alitaja namba yake ya usahili baada ya Walinzi kujiridhisha walimpa kitambulisho akaingia ndani.
Alijiamini kupita maelezo....alikaa kwenye kiti kisha akakunja nne
"Elon...." Kijana mmoja aliyekuwa karibu yake alimuita
Ava ndio kushtuka koti la alilovaa limeandikwa jina la Kaka yake.
"Hakuwa na haja ya kuandika majina nguo zake" Ava alijisemea kisha akajiweka bize, hakuwa tayari kuzungumza chochote na Mwanaume huyu
Akiwa hapa ametulia alimuona Elon kwa mbali akiwa kabeba pochi ya Katarina. Alifumba na kufumbua lakini hakumuona tena....aliamini wenge ndio lina msumbua lakini ukweli ni kwamba macho yake yalikuwa sahihi
Tangazo lilitolewa watu wote wasimame kwa ajili ya kumkaribisha CEO wa Kampuni ya Penfolds.
Macho ya Ava yalishtuka baada ya kumuona Easton akiwa na jopo la watu waliovaa suti kali pamoja na vitambulisho shingoni mwao
*04*
"Nimefurahi kuona nyie wote hapa mpo kwa nia ya kufanya kazi na Mimi.... huenda wengi wenu mkawa hamnifahamu, naitwa Easton ni CEO wa hili Kampuni" Easton aliongea kisha akaachia tabasamu
"Laiti ningejua huyu panya ndio CEO wa hili Kampuni nisingeji sumbua kutuma maombi" Ava aliongea pekee yake akionekana kukata tamaa
"Easton si mtu wa kuendeshwa na migogoro binafsi....sijui ni kitu gani umemkosea lakini usivunjike moyo kwa sababu hatakukumbusha kosa lako" Binti aliyekuwa amekaa jirani yake alimsaidia kumtoa hofu
"Kosa nililofanya ni la jinai, siwezi kuamini katika matumaini yako" Ava aliongea
"Kitu pekee ambacho hawezi kusamehe ni udanganyifu tena katika mapenzi....kuwa na amani" Binti huyu alizungumza....ni wazi kabisa kabla ya kuja kwenye usahili alifatilia sifa za Mwajiri wake
Ava alikaa kwa kutulia baada ya Binti huyu kumpa matumaini.
Baada ya watu wote kupata chai, usahili ulianza.
Asilimia kubwa ya watu waliamini katika uwezo wao, tofauti na Ava aliamini katika tambiko alilofanya pamoja na mkufu aliovaa.
Hatimaye aliitwa katika chumba cha usahili.
Moyo wake ulilipuka zaidi baada ya kukutana macho na Easton.
Yule Binti alikuwa sahihi, Easton alionesha dalili zote za kutomfahamu Ava.
"Nahitaji kusikia ni kitu gani utafanya kuhusu Kampuni letu pindi utakapopata nafasi" Easton aliuliza
"Nitafanya vitu vilivyo nje ya uwezo wangu" Ava alijibu
Watu wote walimshangaa kwa jibu lake, Easton alimpa ishara aelezee maana ya jibu lake
"Nitahakikisha nafanya maamuzi magumu kuliokoa Kampuni endapo litakuwa katika wakati mgumu..." Ava aliongea
Secretary Jo alimruhusu aondoke, ni wazi hakufurahishwa na majibu yake hivyo aliweka alama x kwenye jina la Ava.
Baada ya usahili kumalizika, Secretary Jo aliwasogelea wasahili wote
"Nipo hapa kwa niaba ya CEO, tunashukuru kwa ushirikiano wenu mzuri, leo saa sita kamili usiku kila mtu aingie kwenye email yake kuona matokeo ya alichofanya, kuanzia sasa na kuendelea naomba msipige simu wala kuja ofisini kuulizia majibu kwani kila kitu kitamalizika kwenye email" Secretary Jo aliongea kisha akaondoka
Mapigo ya moyo wa Ava yalikuwa juu sana, ni wazi hakuwa na uhakika na kitu alichokifanya.... alijikuta akivua koti la Kaka yake baada ya kuhisi joto. Akiwa anatembea taratibu macho yake yalitua kwenye kioo kilichokuwa ukutani....alijicheka mwenyewe kwa namna alivyoonekana kituko kwa mavazi aliyovaa.
Upande wa Penfolds alianza kupitia majina ya watu walionekana kufanya vizuri....alimtazama kwa macho makubwa Secretary Jo baada ya jina la Ava kuonekana limewekwa mkasi
"Namkumbuka huyu binti vizuri, nguo alizokuwa amevaa pamoja na viatu vinatosha kumuonesha hana nidhamu..... muonekano wake ni mbaya, kitu kingine kilicho muangusha ni aina ya jibu alilotoa, ni kama anatamaa ya kuwa CEO na si Mfanyakazi" Secretary Jo aliongea
"Kwa upande wangu anafaa, ni watu wachache sana wanaweza kufikiria kufanya maamuzi magumu kuhusu Kampuni ambalo si lake, na kuhusu muonekano hivyo ndivyo alivyo watu wengi wamekuja na mionekano bandia lakini yeye kajikubali alivyo, hivyo nampitisha.... hakikisha siku ya kesho anafika hapa ofisini kuanza kazi" Easton aliongea
Secretary Jo alitaka kupinga lakini macho ya Easton yalimnyamazisha.
Ava hakwenda nyumbani badala yake alielekea ufukweni mwa bahari kuu ya Mini, alitandika koti lake akajilaza. Kichwa chake kilikuwa tupu, hakuwa na kitu cha kufikiria zaidi ya kufumba macho.
Baada ya kuchoka kukaa mahali hapa aliondoka akasahau koti
"Koti la Elon...." Ava aliongea pekee yake baada ya kukumbuka
Alirudi ufukweni kwa kukimbia, bahati nzuri au mbaya aliparamiana na Elon (Kaka yake)
"Elon?..." Ava aliita kwa sauti ya uoga asiamini anachokiona
"Umenifananisha pole kwa hilo" Elon aliongea kisha akaondoka
Hakuwa tayari kurudi kwa familia yake sababu ya Katarina, hakuwa tayari kujua watu hawa kwa sasa wanaishije bila yeye kwa sababu ndio alikuwa mhimili mkubwa.
Ava hakutaka kuelewa, alimkimbilia Kaka yake kisha akakagua alama iliyokuwa kwenye mkono.
Machozi yalimdondoka baada ya kugundua mtu huyu ni Kaka yake wa damu kabisa
"Sitakuuliza wala kukuomba urudi nyumbani, nitajifanya sijaona chochote" Ava aliongea kisha akaondoka, hakutaka kufatilia kuhusu mkoti tena
Alifika nyumbani akiwa amelowa machozi, Jessica alimkumbatia binti yake akiwa mwenye hofu
"Elon anaishi...kwa haraka tu ana maisha mazuri, kuanzia sasa na kuendelea acha kumfikiria wala kuumia moyo kisa yeye" Ava aliongea akizidisha kulia
Jessica alikaa kimya hakujua ni maneno gani anapaswa kuongea.
Upande Easton baada ya kurejea nyumbani, aliachia tabasamu kutokana na chakula kilichokuwa mezani.
Hakusubiria kukaribishwa, alikaa akaanza kula
"Tabasamu lako usoni linatosha kuniambia Katarina ni Mpishi vizuri" Selena aliongea
Easton alidondosha kijiko, tabasamu lilipotea usoni mwake
"Kuanzia sasa nitakuwa na kula hotelini.