Simulizi
Member
SIMULIZI: MAMA MKWE MCHAWI
SEHEMU YA KWANZA (01)
"Hivi we mwanamke mie kila siku niwe naongea tu, naongea ili unifanye nionekane mbaya kwa majirani sindio?" Bwana Brison Aidan aliuliza kwa ukali punde baada ya kufunua Hotpot ya chakula alicholetewa na mke wake Bi Paulina, mkewe alistaajabu kwa swali lile aliloulizwa na mume wake hivyo alirudi nakusimama amsikilize tena.
"Mume wangu umesemaje?" Aliuliza Paulina kwa upole huku akimtizima mume wake aliekuwa amekasirika na kukunja sura yake wazi wazi.
"ET MUME WANGU UNASEMAJE?? NA WEWE UNAULIZA KABISA NASEMAJE?? HIKI NINI KWENYE HICHI CHAKULA?? HIZI SI MENDE HIZI! NA UNANIAMBIAGA ETI NAFUNIKAGA, WE UNANIPENDA KWELI UNITENGEE CHAKULA KINA MENDE HIVI?!" bwana Brison aliuliza kwa ukali huku akiibana pua kwa dharau, licha ya kuwa majirani zao walishazizoea kelele zile lakini siku hiyo zilipenya sana hata jirani yake mmoja aliposikia maneno yale alisongea akalitege sikio, ingawaje ilikuwa ni usiku wa saa mbili ambapo bwana Brison alikuwa amerudi kutoka kazini kwake.
"Lakini mume wangu mie siwezi kukutengea mende kwa lipi baya mume wangu ulilolifanya mpaka mimi nikulipe kwa baya kiasi hicho! nisamehe mume wangu sikujua kama waliingia mende kwenye hotpot ya chakula" Paulina alishuka chini na kupiga goti akimuomba mumewe amsamehe kosa lake kwani alihisi kuwa ni udhaifu wake ndio umepelekea vile.
"UNITOKEE HAPA KWANZA UMENINYIMA WATOTO HADI LEO HUZAI WEWE MWANAMKE GANI SASA! YANI NAJUTA HATA KUKUOA KABISA UMEKALIA KULIA TU INAFAIDA GANI KULIA? UKITAKA KULIA LIAA MWANA KULIA NA WE NGOJA TU!" Brison aliongea kwa hasira na. kuisukuma Hotpot ya chakuka kwa hasira kisha akanyanyuka mezani na kwenda zake chumbani.
Alimuacha mkewe bi Paulina akilia maskini kutokana na ugumba alionao kutopata mtoto tu ndio chanzo cha mume wake kumuona hafai, kwani ni miaika takribani mitatu toka wafunge pingu za maisha mbele ya kanisa kubwa kabisa liliohudhuriwa na waumini kibao siku hiyo, Toka wafunge ndoa hiyo hakufanikiwa kupata mtoto au hata mimba kuharibika licha ya kuwa mumewe alijitahidi kumtimizia hitaji la ndoa kila siku, alilia sana Hidaya huku akinyanyua mikono yake juu na kumuomba mola wake amjaalie apate japo mtoto hata mmoja ili ndoa yake iwe na furaha isiwe kama hivyo anavyotaabika, aliongea kwa huruma huku machozi yakiuchakaza uso wake wa urembo na kuiweka sura nyekundu kwa simanzi.
"Eeh! Mungu wangu niondolee balaa hili, kisa ugumba wangu mume wangu ananisimanga! hanipendi tena, eeh! Mungu nionee huruma na mie nifanye niitwe mama mungu wangu!! Nitaishi hivi hadi lini? najua Mungu unaniona na kunisikia nijibu Mungu wangu" Aliongea Paulina huku akilia sana alishusha maombi mazito Mungu amjaalie angalau abahatike hata kupata mtoto mmoja ili amfurahishe mume wake, Akiwa amebaki mwenyewe sebleni alisikia sauti ya mlango ukipigwa kwa nje huku ikifatia na sauti ikiita.
"Wa humu! Paulina! Paulina" taratibu alifuta machozi na kujikongoja kwenda ulipo mlango na kuufungua, na hapo alikutana na sura ya mzee aliekuwa pale mlangoni.
"Aah!! mjumbe!!" Paulina aliguna na kujibaraguza mjumbe asigundue kama alikuwa analia.
"Kuna usalama hapa?" mjumbe aliuliza huku akipitisha macho kwa ndani.
"Ndio mzee wangu tena wakutosha tu" Paulina alijikakamua na kuficha maumivu yake kisha akamjibu kama vile hakuwa analia mda mfupi uliopita.
"Nimesikia kelele kelele nikajua labda usalama utakuwa mdogo nikaona bora nije nichungulie jirani" Mjumbe aliongea huku safari hii akimtizama Paulina kuanzia juu mpaka chini.
"Usalama upo wa kutosha mzee wangu yani usiwe na wasiwasi" Paulina alijibu bado akiendelea kuweka siri kwa tukio liliotokea.
"Basi kama kuna usalama mie nirudi kwangu" Mjumbe aliongea kisha akamuaga Paulina nae mjumbe akaelekea kwake.
"Nfyuuu!! Baba zima ovyo umbea tu mambo ya watu we yanakuhusu nini kwenda huko" Paulina alifyonya kisha akaufunga mlango na kwenda moja kwa moja kwa mumewe, Brison alikuwa amejitupia kitandani na nguo zake zile zile alizovaa na kushinda nazo kazini, hakuwa na mda wa kufikiria kuvua viatu au kubadilisha nguo zile, Paulina alipomuona mumewe yuko katika hali ile hakupenda kabisa, na moyo wake ulimuua sana kwani hakupenda kumuona mumewe akiwa hana furaha.
"Mume wangu usiwe mnyonge kiasi hicho unanitia simanzi na mimi, mtoto ni rehma za Mungu tutampata tu isikupe..."
"NITOLEE KELELE ZAKO HAPA USHANICHOSHA, TUTAPATA TUTAPATA MBONA HATUPATI SASA, IMEKUWA KILA SIKU NYIMBO ILE ILE TUTAPATA USINIGUSE TENA!" Brison aliongea kwa ukali kisha akageukia pembeni na kumtegea mgongo Paulina, Paulina alitizama hali ile alichukulia ni sehemu katika maisha yake na mume wake ndio hivyo alivyoamua, alitingisha kichwa na kushuka kitandani kisha akabadilisha nguo zake na kurudi tena kitandani ili amvue zile nguo mumewe, lakini siku hiyo Brison alikuwa mkali kupitiliza hakutaka hata kuguswa na mkewe ingawaje ni mke halali wa ndoa.
"WE UPENDO WAKO NIKUNIBADILISHA NGUO? NIACHE UKINIGUSA TENA NITAKUPASUA" alisema Brison.
"Sawa mume wangu ni hayo tu basi ulale salama" Paulina aliongea na kuuvuta upande wa shuka na kumfunika mumewe lakini mumewe aliufunua na kukaa kitandani hakutaka kabisa kujumuika nae kwa siku hiyo.
"Unaenda wapi mume wangu?" Paulina alishtuka baada ya kumuona mume wake akibadilisha shati na kuvaa lingine kisha juu yake akavalia sweta.
"WE HAIKUHUSU!!" Brison alijibu na kutoka ndani, Paulina aliamka na kumuangaza mumewe hakumuona tena alilia sana maskini! alikaa nje kumsubiri mumewe arudi hadi saa saba kasoro akiwa chakula cha mbu nje lakini wapi Brison hakulala kabisa nyumbani hapo, Paulina alirudi ndani kwa unyonge na kuufunga mlango akajifunika shuka huku akiwa amekumbatia picha ya mumewe aliempenda kwa dhati Brison.
"Eeh! Mungu wangu uangazie mkono wako wa ulinzi kwa mume wangu arudi salama" licha ya kupitia misuko suko mingi kwenye ndoa yake lakini Paulina alizidi kumpenda mume wake hakuona sababu ya kumrudishia baya ingali anahaki kama mume, alimuombea dua mumewe kisha akajilaza, akiwa amekumbatia picha iliopigwa siku ya harusi yao.
Baada ya bwana Brison kutoka Nyumbani kwake alikodi boda boda hadi Mtaa wa Marimbe, moja kwa moja alifikishwa kweye nyumba ndogo alioitenga Brison na kwenye nyumba hiyo alimpa hifadhi mwanamke wa nje (Hawara) mwanamke huyo aliitwa Ziada, Ziada ni mwanamke tu waliefahamiana kwa mda mfupi tena bar ambako Ziada alikuwa akifanya kazi ya uhudumu, lakini si! uhudumu tu alikuwa anacheo pia kwenye bar hiyo baada ya mda alipewa cheo nakuwa 'Kaunta' kabla ya kuwekwa kimada na Brison, usiku huo Brison alifika kwa Ziada na kumgongea mlango nae Ziada hakuwa amelala hivyo aliamka na kufungulia kwa bashasha, "wow! mume wangu umerudi?" Ziada alimlaki hawara wake akimuonyesha mapenzi ya kweli, nae Brison alijiona kutulia kabisa akiwa na Ziada mwanamke wa nje kuliko hata Paulina mke halali kabisa.
"Aagh! lile limwanamke lishenzi kweli limenikera huko we acha tu" Brison alijibu huku wakivuta meza na kukaa pamoja kisha Ziada akaleta chakula na kukitenga pale Mezani.
"Yaani niliwaza sana kama utalala huko! nisingeweza kula kabisa" Ziada aliongea na kuchukua jagi la maji ya uvugu vugu na kumwagilia Brison anawe mikono ili wapate chakula, Brison alinawa na baada ya yote Hotpot ikafunguliwa na wakaanza kuumega ugari wa baridi na dagaa, Brison alivutika sana na ugari aliopata kwa Ziada kuliko chakula alichoandaliwa na mke wake Paulina, hakukumbuka kabisa kama ni mke wake wa ndoa, kule mwenzake alimuacha analia huku yeye anasherehekea na hawara aliemkwapua bar majuma matatu yaliyopita.
***********************
Walipomaliza kula walipanda kitandani kulala, huku stori za hapa na pale zikiwatawala wapenzi hao.
"Daah! hivi lini nitakuwa mke wako?" Ziada alianza kwa kuuliza huku akikichezea kifua cha Brison, Brison alikuwa kimya kwa mda kisha akamjibu.
"aahgh! hilo niachie mimi yani ni siku yeyote ile nataka kwanza nimtimue yule, mwanamke gani hajitambui" Brison aliongea na kumponda mke wake mbele ya hawara wake.
"Si umfukuze tu kama hajielewi" Ziada aliongea kumchochea hasira Brison, aliposikia kauli ile Brison aliona ni wazo zuri alilopewa na Ziada.
"Halafu kweli ngoja sikulijua mapema yule natimua halafu nakuoa wewe tunaishi kwa amani kabisa" Brison aliongea na kumpa matumaini Ziada ya kumuoa, walilala kwa kukumbatiana kimahaba mpaka asubuhi ya Jumamosi ilipofika, kama kawaida ya siku hiyo wafanyakazi wengi hupumzika katika siku hizo mbili, hivyo siku hiyo bwana Brison Aidan hakwenda kazini.
********************************
Aliamka asubuhi nakutoka nje huku ndani akimuacha Ziada bado akikumbatia shuka kwa ubaridi ule wa Asubuhi, alikaa kwenye msingi wa Nyumba hiyo huku akiwa ni mwingi wa mawazo, na kubwa zaidi lililomuumiza kichwa ni juu ya muafaka juu ya mke wake Paulina.
"Hazai! kweli kama hana mbegu mie wanini huyu? mie sio muislam kusema nioe mke wa pili, sasa ni hivi namtimua arudi kwao, acha nimuoe Ziada kwanza isitoshe Ziada ana mtoto mmoja hivyo nitapanda nae mbegu" aliwaza Brison kwa mda, alipokamilisha mipango yake alikung'uta vumbi na kurudi ndani, alimkuta Ziada akiwa ameshaamka na tayari alikuwa anamalizia kutandika kitanda, alisogea taratibu na kumkumbatia kwa nyuma huku mikono yake ikikutana kati kati tumboni.
"Aah!! mi naona niondoke niende huko nikamtimue huyo mwanamke" Brison alizungumza huku kichwa chake akiwa amekilaza juu ya mgongo wa mwanadada huyo.
"Kweli???" Ziada aligeuka haraka na kumuuliza kwa mshituko huku sura na moyo wake vikitandwa kwa furaha ya kusikia lile.
"Ndio natimulia mbali na wewe ndio utashika usukani wote" Brison aliongea na kumpa uhakika Ziada.
"Ndio maana nakupendaga mwaaaaah!!" Ziada aliongea kwa furaha na kumpiga busu Brison busu lilimchanganya zaidi na kumfanya awaze maamuzi mabaya tu mbele yake, alimkumbatia Ziada kwa nguvu kisha wakaachana, alitoka nje na kupanda boda boda tena iliomuokolea muda kufika kwake, alifika na kupitiliza ndani bila ya salamu ingali Mkewe alikuwepo nje akimfulia nguo zake.
"Mume wangu umerudi?" Paulina alipomuoana mume wake aliacha kufua na kumfata mume wake ndani alipoingia kwa fujo, lakini Brison alikuwa kama hamsikii ingawaje aliondoka usiku wa jana.
"Mume wangu! mume wangu! mbona uko hivyo lakini!" Paulina aliongea kwa sauti kumsimamisha mume wake lakini bwana Brison hakuwa hiari kusimama aliingia chumbani kwao na kuanza kuchagua nguo kwa kuzitenga zake na za Paulina.
"MUME WANGU UNAFANYAJE MBONA SIKUELEWI??" Paulina aliuliza baada ya kuona mumewe akivuruga amani ndani mle.
"WE NANI MUME WAKO? MI SINA MKE" Brison alijibu kwa ukali huku akiendelea kutoa vitu ovyo ovyo!
"Lakini Mume wangu!!!" kabla hajaongea kitu chochote Paulina, Brison alimzuia kwa kofi zito, kofi liliomplekea Paulina kukaa kimya kabisa.
"NIMESHAKWAMBIA UNYAMAZE!!" alimsukumizia neno huku akimtizama kwa jicho kali, Paulina alishika shavu na kuendelea kulia maskini! Nguo zote za Paulina zilizokuwa kwenye begi Brison alizitoa zote na kumfungia kwenye vitenge vyake mafurushi matatu kisha akatoka nje na. kumtupia.
"NGUO ZAKO ZISHATANGULIA NJE NA WEWE UTOKE HAPA!" Brison alirudi ndani na kuongea huku akimsukuma Paulina mgongoni atoke nje.
"KOSA LANGU NINI??" Paulina aliuliza
"SITAKI KELELE TOKA HAPA" Brison aliongea kwa ukali.
ITAENDELEA.....
We unafikiri Bwana Brison ameamua haki kumfukuza Paulina kisa Ziada??
SEHEMU YA KWANZA (01)
"Hivi we mwanamke mie kila siku niwe naongea tu, naongea ili unifanye nionekane mbaya kwa majirani sindio?" Bwana Brison Aidan aliuliza kwa ukali punde baada ya kufunua Hotpot ya chakula alicholetewa na mke wake Bi Paulina, mkewe alistaajabu kwa swali lile aliloulizwa na mume wake hivyo alirudi nakusimama amsikilize tena.
"Mume wangu umesemaje?" Aliuliza Paulina kwa upole huku akimtizima mume wake aliekuwa amekasirika na kukunja sura yake wazi wazi.
"ET MUME WANGU UNASEMAJE?? NA WEWE UNAULIZA KABISA NASEMAJE?? HIKI NINI KWENYE HICHI CHAKULA?? HIZI SI MENDE HIZI! NA UNANIAMBIAGA ETI NAFUNIKAGA, WE UNANIPENDA KWELI UNITENGEE CHAKULA KINA MENDE HIVI?!" bwana Brison aliuliza kwa ukali huku akiibana pua kwa dharau, licha ya kuwa majirani zao walishazizoea kelele zile lakini siku hiyo zilipenya sana hata jirani yake mmoja aliposikia maneno yale alisongea akalitege sikio, ingawaje ilikuwa ni usiku wa saa mbili ambapo bwana Brison alikuwa amerudi kutoka kazini kwake.
"Lakini mume wangu mie siwezi kukutengea mende kwa lipi baya mume wangu ulilolifanya mpaka mimi nikulipe kwa baya kiasi hicho! nisamehe mume wangu sikujua kama waliingia mende kwenye hotpot ya chakula" Paulina alishuka chini na kupiga goti akimuomba mumewe amsamehe kosa lake kwani alihisi kuwa ni udhaifu wake ndio umepelekea vile.
"UNITOKEE HAPA KWANZA UMENINYIMA WATOTO HADI LEO HUZAI WEWE MWANAMKE GANI SASA! YANI NAJUTA HATA KUKUOA KABISA UMEKALIA KULIA TU INAFAIDA GANI KULIA? UKITAKA KULIA LIAA MWANA KULIA NA WE NGOJA TU!" Brison aliongea kwa hasira na. kuisukuma Hotpot ya chakuka kwa hasira kisha akanyanyuka mezani na kwenda zake chumbani.
Alimuacha mkewe bi Paulina akilia maskini kutokana na ugumba alionao kutopata mtoto tu ndio chanzo cha mume wake kumuona hafai, kwani ni miaika takribani mitatu toka wafunge pingu za maisha mbele ya kanisa kubwa kabisa liliohudhuriwa na waumini kibao siku hiyo, Toka wafunge ndoa hiyo hakufanikiwa kupata mtoto au hata mimba kuharibika licha ya kuwa mumewe alijitahidi kumtimizia hitaji la ndoa kila siku, alilia sana Hidaya huku akinyanyua mikono yake juu na kumuomba mola wake amjaalie apate japo mtoto hata mmoja ili ndoa yake iwe na furaha isiwe kama hivyo anavyotaabika, aliongea kwa huruma huku machozi yakiuchakaza uso wake wa urembo na kuiweka sura nyekundu kwa simanzi.
"Eeh! Mungu wangu niondolee balaa hili, kisa ugumba wangu mume wangu ananisimanga! hanipendi tena, eeh! Mungu nionee huruma na mie nifanye niitwe mama mungu wangu!! Nitaishi hivi hadi lini? najua Mungu unaniona na kunisikia nijibu Mungu wangu" Aliongea Paulina huku akilia sana alishusha maombi mazito Mungu amjaalie angalau abahatike hata kupata mtoto mmoja ili amfurahishe mume wake, Akiwa amebaki mwenyewe sebleni alisikia sauti ya mlango ukipigwa kwa nje huku ikifatia na sauti ikiita.
"Wa humu! Paulina! Paulina" taratibu alifuta machozi na kujikongoja kwenda ulipo mlango na kuufungua, na hapo alikutana na sura ya mzee aliekuwa pale mlangoni.
"Aah!! mjumbe!!" Paulina aliguna na kujibaraguza mjumbe asigundue kama alikuwa analia.
"Kuna usalama hapa?" mjumbe aliuliza huku akipitisha macho kwa ndani.
"Ndio mzee wangu tena wakutosha tu" Paulina alijikakamua na kuficha maumivu yake kisha akamjibu kama vile hakuwa analia mda mfupi uliopita.
"Nimesikia kelele kelele nikajua labda usalama utakuwa mdogo nikaona bora nije nichungulie jirani" Mjumbe aliongea huku safari hii akimtizama Paulina kuanzia juu mpaka chini.
"Usalama upo wa kutosha mzee wangu yani usiwe na wasiwasi" Paulina alijibu bado akiendelea kuweka siri kwa tukio liliotokea.
"Basi kama kuna usalama mie nirudi kwangu" Mjumbe aliongea kisha akamuaga Paulina nae mjumbe akaelekea kwake.
"Nfyuuu!! Baba zima ovyo umbea tu mambo ya watu we yanakuhusu nini kwenda huko" Paulina alifyonya kisha akaufunga mlango na kwenda moja kwa moja kwa mumewe, Brison alikuwa amejitupia kitandani na nguo zake zile zile alizovaa na kushinda nazo kazini, hakuwa na mda wa kufikiria kuvua viatu au kubadilisha nguo zile, Paulina alipomuona mumewe yuko katika hali ile hakupenda kabisa, na moyo wake ulimuua sana kwani hakupenda kumuona mumewe akiwa hana furaha.
"Mume wangu usiwe mnyonge kiasi hicho unanitia simanzi na mimi, mtoto ni rehma za Mungu tutampata tu isikupe..."
"NITOLEE KELELE ZAKO HAPA USHANICHOSHA, TUTAPATA TUTAPATA MBONA HATUPATI SASA, IMEKUWA KILA SIKU NYIMBO ILE ILE TUTAPATA USINIGUSE TENA!" Brison aliongea kwa ukali kisha akageukia pembeni na kumtegea mgongo Paulina, Paulina alitizama hali ile alichukulia ni sehemu katika maisha yake na mume wake ndio hivyo alivyoamua, alitingisha kichwa na kushuka kitandani kisha akabadilisha nguo zake na kurudi tena kitandani ili amvue zile nguo mumewe, lakini siku hiyo Brison alikuwa mkali kupitiliza hakutaka hata kuguswa na mkewe ingawaje ni mke halali wa ndoa.
"WE UPENDO WAKO NIKUNIBADILISHA NGUO? NIACHE UKINIGUSA TENA NITAKUPASUA" alisema Brison.
"Sawa mume wangu ni hayo tu basi ulale salama" Paulina aliongea na kuuvuta upande wa shuka na kumfunika mumewe lakini mumewe aliufunua na kukaa kitandani hakutaka kabisa kujumuika nae kwa siku hiyo.
"Unaenda wapi mume wangu?" Paulina alishtuka baada ya kumuona mume wake akibadilisha shati na kuvaa lingine kisha juu yake akavalia sweta.
"WE HAIKUHUSU!!" Brison alijibu na kutoka ndani, Paulina aliamka na kumuangaza mumewe hakumuona tena alilia sana maskini! alikaa nje kumsubiri mumewe arudi hadi saa saba kasoro akiwa chakula cha mbu nje lakini wapi Brison hakulala kabisa nyumbani hapo, Paulina alirudi ndani kwa unyonge na kuufunga mlango akajifunika shuka huku akiwa amekumbatia picha ya mumewe aliempenda kwa dhati Brison.
"Eeh! Mungu wangu uangazie mkono wako wa ulinzi kwa mume wangu arudi salama" licha ya kupitia misuko suko mingi kwenye ndoa yake lakini Paulina alizidi kumpenda mume wake hakuona sababu ya kumrudishia baya ingali anahaki kama mume, alimuombea dua mumewe kisha akajilaza, akiwa amekumbatia picha iliopigwa siku ya harusi yao.
Baada ya bwana Brison kutoka Nyumbani kwake alikodi boda boda hadi Mtaa wa Marimbe, moja kwa moja alifikishwa kweye nyumba ndogo alioitenga Brison na kwenye nyumba hiyo alimpa hifadhi mwanamke wa nje (Hawara) mwanamke huyo aliitwa Ziada, Ziada ni mwanamke tu waliefahamiana kwa mda mfupi tena bar ambako Ziada alikuwa akifanya kazi ya uhudumu, lakini si! uhudumu tu alikuwa anacheo pia kwenye bar hiyo baada ya mda alipewa cheo nakuwa 'Kaunta' kabla ya kuwekwa kimada na Brison, usiku huo Brison alifika kwa Ziada na kumgongea mlango nae Ziada hakuwa amelala hivyo aliamka na kufungulia kwa bashasha, "wow! mume wangu umerudi?" Ziada alimlaki hawara wake akimuonyesha mapenzi ya kweli, nae Brison alijiona kutulia kabisa akiwa na Ziada mwanamke wa nje kuliko hata Paulina mke halali kabisa.
"Aagh! lile limwanamke lishenzi kweli limenikera huko we acha tu" Brison alijibu huku wakivuta meza na kukaa pamoja kisha Ziada akaleta chakula na kukitenga pale Mezani.
"Yaani niliwaza sana kama utalala huko! nisingeweza kula kabisa" Ziada aliongea na kuchukua jagi la maji ya uvugu vugu na kumwagilia Brison anawe mikono ili wapate chakula, Brison alinawa na baada ya yote Hotpot ikafunguliwa na wakaanza kuumega ugari wa baridi na dagaa, Brison alivutika sana na ugari aliopata kwa Ziada kuliko chakula alichoandaliwa na mke wake Paulina, hakukumbuka kabisa kama ni mke wake wa ndoa, kule mwenzake alimuacha analia huku yeye anasherehekea na hawara aliemkwapua bar majuma matatu yaliyopita.
***********************
Walipomaliza kula walipanda kitandani kulala, huku stori za hapa na pale zikiwatawala wapenzi hao.
"Daah! hivi lini nitakuwa mke wako?" Ziada alianza kwa kuuliza huku akikichezea kifua cha Brison, Brison alikuwa kimya kwa mda kisha akamjibu.
"aahgh! hilo niachie mimi yani ni siku yeyote ile nataka kwanza nimtimue yule, mwanamke gani hajitambui" Brison aliongea na kumponda mke wake mbele ya hawara wake.
"Si umfukuze tu kama hajielewi" Ziada aliongea kumchochea hasira Brison, aliposikia kauli ile Brison aliona ni wazo zuri alilopewa na Ziada.
"Halafu kweli ngoja sikulijua mapema yule natimua halafu nakuoa wewe tunaishi kwa amani kabisa" Brison aliongea na kumpa matumaini Ziada ya kumuoa, walilala kwa kukumbatiana kimahaba mpaka asubuhi ya Jumamosi ilipofika, kama kawaida ya siku hiyo wafanyakazi wengi hupumzika katika siku hizo mbili, hivyo siku hiyo bwana Brison Aidan hakwenda kazini.
********************************
Aliamka asubuhi nakutoka nje huku ndani akimuacha Ziada bado akikumbatia shuka kwa ubaridi ule wa Asubuhi, alikaa kwenye msingi wa Nyumba hiyo huku akiwa ni mwingi wa mawazo, na kubwa zaidi lililomuumiza kichwa ni juu ya muafaka juu ya mke wake Paulina.
"Hazai! kweli kama hana mbegu mie wanini huyu? mie sio muislam kusema nioe mke wa pili, sasa ni hivi namtimua arudi kwao, acha nimuoe Ziada kwanza isitoshe Ziada ana mtoto mmoja hivyo nitapanda nae mbegu" aliwaza Brison kwa mda, alipokamilisha mipango yake alikung'uta vumbi na kurudi ndani, alimkuta Ziada akiwa ameshaamka na tayari alikuwa anamalizia kutandika kitanda, alisogea taratibu na kumkumbatia kwa nyuma huku mikono yake ikikutana kati kati tumboni.
"Aah!! mi naona niondoke niende huko nikamtimue huyo mwanamke" Brison alizungumza huku kichwa chake akiwa amekilaza juu ya mgongo wa mwanadada huyo.
"Kweli???" Ziada aligeuka haraka na kumuuliza kwa mshituko huku sura na moyo wake vikitandwa kwa furaha ya kusikia lile.
"Ndio natimulia mbali na wewe ndio utashika usukani wote" Brison aliongea na kumpa uhakika Ziada.
"Ndio maana nakupendaga mwaaaaah!!" Ziada aliongea kwa furaha na kumpiga busu Brison busu lilimchanganya zaidi na kumfanya awaze maamuzi mabaya tu mbele yake, alimkumbatia Ziada kwa nguvu kisha wakaachana, alitoka nje na kupanda boda boda tena iliomuokolea muda kufika kwake, alifika na kupitiliza ndani bila ya salamu ingali Mkewe alikuwepo nje akimfulia nguo zake.
"Mume wangu umerudi?" Paulina alipomuoana mume wake aliacha kufua na kumfata mume wake ndani alipoingia kwa fujo, lakini Brison alikuwa kama hamsikii ingawaje aliondoka usiku wa jana.
"Mume wangu! mume wangu! mbona uko hivyo lakini!" Paulina aliongea kwa sauti kumsimamisha mume wake lakini bwana Brison hakuwa hiari kusimama aliingia chumbani kwao na kuanza kuchagua nguo kwa kuzitenga zake na za Paulina.
"MUME WANGU UNAFANYAJE MBONA SIKUELEWI??" Paulina aliuliza baada ya kuona mumewe akivuruga amani ndani mle.
"WE NANI MUME WAKO? MI SINA MKE" Brison alijibu kwa ukali huku akiendelea kutoa vitu ovyo ovyo!
"Lakini Mume wangu!!!" kabla hajaongea kitu chochote Paulina, Brison alimzuia kwa kofi zito, kofi liliomplekea Paulina kukaa kimya kabisa.
"NIMESHAKWAMBIA UNYAMAZE!!" alimsukumizia neno huku akimtizama kwa jicho kali, Paulina alishika shavu na kuendelea kulia maskini! Nguo zote za Paulina zilizokuwa kwenye begi Brison alizitoa zote na kumfungia kwenye vitenge vyake mafurushi matatu kisha akatoka nje na. kumtupia.
"NGUO ZAKO ZISHATANGULIA NJE NA WEWE UTOKE HAPA!" Brison alirudi ndani na kuongea huku akimsukuma Paulina mgongoni atoke nje.
"KOSA LANGU NINI??" Paulina aliuliza
"SITAKI KELELE TOKA HAPA" Brison aliongea kwa ukali.
ITAENDELEA.....
We unafikiri Bwana Brison ameamua haki kumfukuza Paulina kisa Ziada??